Mhandisi
Ibrahim Kibasa (kulia) akipata ufafanuzi kutoka kwa Kaimu Meneja wa
Kiwanja cha Ndege cha Iringa, Lydia Mwenisongole (wapili kulia) wakati
alipotembelea banda la maonesho ya Karibu Utalii Kusini la Mamlaka ya
Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), yanayofungwa leo kwenye viwanja vya
Kihesa-Kilolo, na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Ali Hapi Wengine ni Robert
Kisongo (kushoto) mkazi wa Iringa na Afisa Masoko na Biashara wa TAA,
Mbura Daniel.
Wazee
wa Kimila wa Mkoa wa Iringa kuanzia kulia Anthony Mbuta, Augustino Mkini
na Kassian Ngenz wakiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa Mamlaka ya
Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), baada ya kutembelea banda la maonesho ya
Karibu Utalii Kusini la Mamlaka hiyo, yaliyofungwa leo na Mkuu wa Mkoa wa
Iringa, Mhe. Ali Hapi. Maonesho hayo yalifanyika kwenye viwanja vya
Kihesa-Kilolo mkoani Iringa.
Mhandisi
Astelius John (wa pili kushoto) akimpa maelezo mbalimbali yanayohusu
viwanja vya ndege Tanzania vilivyopo chini ya serikali, Wingred Nkoma,
wakati alipotembelea banda la maonesho ya Karibu Utalii Kusini la mamlaka
hiyo, yaliyofungwa leo na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Ali Hapi kwenye
viwanja vya Kihesa-Kilolo mkoani Iringa.
Maumivu
Mdegela (mwenye koti) pamoja na watoto wake wakipata maelezo mbalimbali
kutoka kwa Afisa Masoko na Biashara wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege
Tanzania (TAA), wakati walipotembelea banda la maonesho ya Karibu Utalii
Kusini yaliyomalizika leo tarehe 22 Septemba, 2019 kwenye viwanja vya
Kihesa-Kilolo mkoani Iringa. Maonesho hayo yamefungwa na Mkuu wa Mkoa,
Mhe. Ali Hapi.
Mkuu
wa Mkoa wa Iringa, Mhe Ali Hapi (wa
kwanza kulia), pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Mhe Richard Kasesela
wakipata maelezo mbalimbali kutoka kwa Kaimu Meneja wa Kiwanja cha Ndege
cha Iringa, Lydia Mwenisiongole, wakati walipotembelea banda la maonesho
ya Karibu Utalii Kusini la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA).
Maonesho hayo yamefungwa leo na Mhe. Hapi.
No comments:
Post a Comment