Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) Mhe.Said Bakar Jecha, alipowasili katika viwanja vya Ukumbiu wa Dk.Ali Mohamed Shein, Tunguu SUZA Wilaya ya Kati Unguja, kusho Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar Dk.Zakia Mohammed Abubakar, na Spika wa Baraza la Wawakiloishi Zanzibar Mhe. Zuberi Ali Maulid.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana Viongozi mbalimbali alipowasili katika viwanja vya Ukumbiu wa Dk.Ali Mohamed Shein, Tunguu SUZA Wilaya ya Kati Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Mwanafunzi wa Chuo Cha Afya Mbweni Kampasi ya SUZA, akitowa maelezo jinsi ya utunzaji wa Afya ya meno, wakati akitembelea maonesho hayo yaliofanyika katika ukumbi wa Dk. Ali Mohamed Shein Tunguu SUZA Wilaya ya Kati Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza mtunza Maktaba (Mkutubi) Ndg. Mohammed Khamis, wakati wa maonesho hayo ya SUZA kusherehekea mafanikio yake tangu kuaziushwa mwaka 1999 hadi 2019, yaliofanyika katika ukumbi wa Dk. Ali Mohamed Shein Tunguu Unguja Wilaya ya Kati.
No comments:
Post a Comment