Kaimu Meneja wa Kiwanja cha Ndege cha Iringa, Lydia Mwenisongole (kushoto) akifafanua mambo mbalimbali yanayohusu Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) walipotembelea maonesho ya Karibu Utalii Kusini, yanayofanyika kwenye viwanja vya Kihesa-Kilolo mkoani Iringa.
Na
Mwandishi Wetu
MAMLAKA
ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), imeimarisha usalama kwa abiria, mizigo na
wageni kwenye viwanja vyake vyote 58 inavyovisimamia.
Kaimu
Meneja wa Kiwanja cha Ndege cha Iringa, Lydia Mwenisongole amesema usalama huo
ni pamoja na mashine za ukaguzi wa abiria na mizigo, ambapo ukaguzi unafanywa
kwa umakini na maafisa usalama waliothibitishwa (certified screeners) na Mamlaka
ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA).
“Tunawakaribisha
wageni wa ndani na nje ya nchi kutumia viwanja vyetu vya ndege kwani vina usalama
wa uhakika, zikiwemo kamera za usalama, X-ray mashine na ukaguzi mwingine
zaidi, ambazo zinafanikisha zoezi zima la usalama,” amesema Mwenisongole.
Mwenisongole
amesema pia tunatambua juhudi za serikali ya Awamu ya Tano, iliyopo chini ya
Mh. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kupitia TAA inampango wa kujenga uzio kwenye
kiwanja cha ndege cha Iringa, ambapo zabuni imeshatangazwa ili kupatikana kwa
mkandarasi wa ujenzi huo.
Pia
amewaita wawekezaji kuwekeza kwenye viwanja vya ndege kwa kuwekeza kwenye
maduka yenye bidhaa mbalimbali pamoja, hoteli na karakana za ndege.
Naye
Mhandisi Astelius John amesema TAA imefanya maboresho makubwa kwenye viwanja
vya ndege kikiwemo kiwanja cha ndege cha Iringa, ambapo kumefanyiwa upanuzi wa
jengo la abiria na ukarabati wa barabara ya kutua na kuruka kwa ndege.
“Tunaboresha
viwanja vya ndege ili viweze kuwa bora na kuhudumia abiria wengi wa ndani na
nje ya nchi kwa lengo la kukuza uchumi wa taifa na sasa kwa Kiwanja cha Ndege
Iringa hii ni kutokana na maboresho ya jengo la abiria kubwa
ambalo lina uwezo wa kuhudumia abiria
wanaotumia kiwanja cha Iringa kutoka 35 kwa siku hadi kufikia 200,” amesema.
Kwa
upande wake Afisa Usalama, Miyaga Juma ametoa ushauri kwa wananchi na wageni
kutoka ndani na nje ya nchi watumie Kiwanja cha ndege cha Iringa, kwani kina usalama
madhubuti, kazi inayofanywa na Maafisa usalama wenye kufuata miongozo
mbalimbali ya kiusalama, aidha TAA imenunua mashine ya kisasa ya Ukaguzi ili kurahisisha
ukaguzi na kuwepo kwa mfumo wa kamera (CCTV) ambao unahifadhi kumbukumbu za
matukio hali inayoboresha usalama Kiwanjani.
No comments:
Post a Comment