Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Wazee wa CCM Wilaya ya Chakechake katika ukumbi wa Kiwanda cha Makonyo Wawi,akiwa Kisiwani Pemba kwa ziara.
RAIS wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, ambaye
pia, ni Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar amesema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar itaendelea kuwatunza na kuwaenzi wazee.
Dk. Shein aliyasema hayo leo huko katika ukumbi wa Kiwanda
cha Mafuta na Makonyo Wawi Mkoa wa Kusini Pemba wakati alipofanya mkutano na
Wazee wa CCM wa Wilaya ya Chake Chake.
Rais Dk. Shein alisema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar inathamini na inazijali juhudi za wazee walizozichukua hadi kupelekea
kupatikana uhuru wa Tanganyika na uhuru wa Zanzibar kupitia vyama vya ASP na
TANU.
Katika hotuba yake aliyoitoa mbele ya wazee hao wa CCM
pamoja na viongozi wengine wakuu wa chama hicho Rais Dk. Shein alisema kuwa wazee
ndio walioijenga Zanzibar na kuleta ukombozi na kuwakomboa wanyonge.
Rais Dk. Shein alitumia fursa hiyo kuwapongeza wazee walioipigania
Zanzibar na hadi hivi leo Zanzibar kuweza kupiga hatua na kupata maendeleo
makubwa.
“Hapa tulipofika ni nguvu za Mwenyezi Mungu pamoja na Wazee
wetu, hivyo pia, yunapongezana kwa kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka
2015 -2020 kuna mengi tumeyafanya na sote tumeshiriki kikamilifu”, alisema Dk.
Shein.
Aidha, Rais Dk. Shein alieleza kuvutiwa na taarifa ya wazee
hao waliyoisoma huku akieleza kuwa ahadi zote zilizoahidiwa na chama hicho zitatekelezwa
hatua kwa hatua.
Makamu Mwenyekiti huyo wa CCM Zanzibar alieleza kuwa
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imekuwa ikitumia wastani wa zaidi ya milioni
600 kwa mwezi kwa ajili ya kuwapa wazee pencheni jamii.
Aliongeza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea
kuchukua juhudi za makusudi katika kuhakikisha wazee wote wanaorodheshwa kwa
ajili ya kupata fedha hizo za pencheni jamii kwa kila mwezi mpaka wale wazee ambao
hawana vyeti vya kuzaliwa.
Alisema kuwa si nchi nyingi duniani zilizo na mfumo huo wa
kuwapa pencheni jamii wazee katika Ukanda wa Afrika Mashariki ni Zanzibar pekee
yenye kufanya utaratibu huo na kusisitiza kuwa kima hicho kilichoanzwa cha elfu
20 si kidogo.
Dk. Shein alieleza namna Serikali ilivyoongeza fedha za
Bajeti kwa Wizara ya Afya kwa ajili ya kununua dawa ambapo hivi sasa vituo
vyote vya afya vya Zanzibar vimekuwa vikipata dawa kwa wakati huku akisisitiza
kuwa endapo akisikia kuna kituo cha afya kinawauzia dawaa wananchi wahusika watashughulikiwa.
Alisema kuwa haiwezekani wananchi wakateseka kwa kukosa
dawa na kueleza kuwa huduma za afya na elimu hapa Zanzibar zitaendelea kuwa
bure na hakuona sababu ya kuanzishwa kwa Bima ya Afya hapa Zanzibar.
Aidha, Makamu Mwenyekiti huyo wa CCM Zanzibar alieleza haja
ya kuwekwa mikakati maalum ya kushughulikia suala zima la unyanyasaji wa
kijinsia hasa kwa watoto wadogo.
Rais Dk. Shein alisisitiza haja kwa WanaCCM kujenga umoja
miongoni mwao kwani umoja wao ndio nguvu zao huku akitumia fursa hiyo kueleza
kuwa Chama hicho ni lazima kiulinde na kuutetea Muungano uliopo.
Alisisitiza haja ya kutumia busara ndani ya chama hicho
sambamba na kuwatumia wazee katika kufanikisha masuala mbali mbali ndani ya
chama hicho kwa maendeleo ya chama na maendeleo ya nchi kwa jumla.
Makamu Mwenyekiti huyo alieleza kuwa ipo haja ya kupokea
mawazo ya wazee sambamba na kuwaheshimu
na kuwalinda wazee kwani kuna kila sababu ya kufanya hivyo hasa ikizingatiwa
historia ya wazee wa nchi hii.
Nae Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Abdalla Juma Mabodi
alisema kuwa hikma za kuwaenzi wazee zimeanza kabda ya Mapinduzi na hadi hivi
leo hikma na busara hizo zinaendelea kutumika ikiwa ni pamoja na kuwatuza wazee
wote wa Unguja na Pemba.
Naibu Mabodi alieleza kuwa ndani ya Chama hicho kuna Mabaraza
ya Wazee ambayo yamekuwa yakisaidia kwa kiasi kikubwa katika kutekeleza
majukumu ya wazee katika kufikia malengo waliyoyakusudia.
Alisema kuwa WanaCCM wana kazi kubwa ya kulinda utamaduni
na silka katika kuilinda Zanzibar ili kuweza kupata mafanikio, uzalendo sambamba
na kuiarisha na kuduisha amani na utulivu uliopo hapa nchini.
Alieleza namna ya kuwatumia kuwa kuwepo kwa wazee na
kuwatumia wazee hao wamekuwa wakikwamaua changamotio kadhaa
Nao Wazee katika taarifa yao walimpongeza kwa kuwapatia
wananchihuduma za kijamii yakiwemo aji safi na salama mjini na vijijini, afya
na elimu bure sambamba na ujenzi wa majengo ya skuli za ghorofa kwa azma ya
kuondosha changamoto zilizopo.
Walieleza mafanikio yaliopatikana ikiwa ni pamoja na ujenzi
wa Matawi, wanafunzi kuendelea kupata elimu bure, vifaa vya kusomea pamoja na ujenzi
wa barabara.
Wazee hao walimpongeza Dk. Shein kwa kusimamia Ilani kwa
kuanzisha utaratibu wa kuwatunza wawzee kwa kuwapatia elfu 20 kwa kila mwezi
bila ya ubaguzi wowote na kueleza jinsi wanavyompongeza Rais Dk. Shein.
Katika taarifa yao hiyo wazee hao walieleza juhudi wanazoendelea
kuzichukua katika kuhakikisha wanaendelea kushikamana ili kuongeza ushindi wa
chama chao.
Wazee hao pia, walieleza changamoto ya matumzi ya dawa za
kulevya pamoja na unyanyasaji wa kijinsia ambao utatokana na matumizi wa dawa za
kulevya jambo ambalo linaondosha silka za Kizanzibari.
Walisisitiza haja ya kuchukuliwa hatua kali za kisheria kwa
yeyote atakaehusika kufanya matukio ya unyanyasaji wa kijinsia.
Nao viongozi wa CCM Wilaya na Mkoa huo wa Kusini Pemba walimpogeza
Dk. Shein kwa jinsi alivyoweza kuwahudumikia wananchi katika kuwatekelezea
huduma za kijamii na kumpongeza Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Dk. John Pombe
Magufuli, kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa SADC na kuahidi kushirikiana nae
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment