Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein. Amtumia Salamu za Pongezi Rais wa China Mhe. Xi Jinping Kwa Kuadhimisha Miaka 70 leo.


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein amemtumia salamu za pongezi Rais wa Jamuhuri ya Watu wa China Mhe.Xi Jinping pamoja na wananchi wa Taifa hilo  kwa kuadhimisha miaka 70 tangu kuundwa kwake.

Katika salamu zake alizotuma kwa Rais Xi Jinping, Dk. Shein amesema kwa niaba ya wananchi na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar anatoa pongezi za dhati kwa Taifa hilo kwa mafanikio makubwa ya kiuchumi na kijamii yaliofikiwa, katika kipindi hicho.

Amesema Zanzibar inajivunia urafiki na uhusiano mzuri wa kihistoria uliopo kati yake na Serikali ya Jamuhuri ya Watu wa China, ikiwa ni matokeo yatokanayo na uongozi bora na uliotukuka kutoka kwa mwasisi wa Taifa hilo Mwenyekiti Mao Zedong.

Aidha amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaunga mkono juhudi zinazoendelea kuchukuliwa na Taifa hilo , ikiwa ni hatua ya kuunga mkono mawazo ya muasisi wake Mweyekiti Mao.

Rais Dk. Shein amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendeleza uhusiano wa kindugu na ushirikano uliopo kati yake na Jamuhuri ya Watu wa China, kwa maslahi ya wananchi wake.

Aidha, Dk. Shein  ametumia fursa hiyo kumtakia afya njema na maisha yenye furaha Rais Xi Jinping  pamoja na wananchi wote wa Taifa hilo.
       
Abdi Shamna, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax: 024 2231822 
 E-mail: abdya062@gmail.com


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.