Wajumbe
wa Bodi ya Zabuni ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wakiwa
katika picha ya pamoja na Wawezeshaji wa seina hiyo eneo la Mtumba katika Mji
wa Serikali leo jijini Dodoma mara baada ya kumaliza mafunzo ya kuwajengea
uwezo wajumbe hao juu ya Sheria ya Ununuzi wa Umma ya mwaka 2011 na marekebisho
yake ya mwaka 2016 pamoja na kanuni zake
za mwaka 2013 ili wawe na usimamizi sahihi wa mikataba yenye kuleta tija na
thamani bora ya fedha za Serikali.
(Picha
na Eleuteri Mangi, WHUSM, Dodoma)
Na
Eleuteri Mangi, WHUSM, Dodoma
Wataalamu
wa Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) wamesitiza Taasisi za Nunuzi kuandaa vizuri mpango wa ununuzi na kusimamia
utekelezaji wake ili mahitaji husika yaweze kununuliwa na kupatikana kwa
wakati.
Akizungumza
na wajumbe wa Bodi ya Zabuni ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
eneo la Mtumba katika Mji wa Serikali jijini Dodoma, Mwezeshaji wa mafunzo
ambaye pia ni Afisa Ununuzi wa Umma kutoka (PPRA) Frank Yesaya amesema nia ya
mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wajumbe hao juu ya Sheria ya Ununuzi wa Umma
ya mwaka 2011 na marekebisho yake ya mwaka 2016 pamoja na kanuni zake ili wawe na usimamizi sahihi wa
mikataba yenye kuleta tija na thamani bora ya fedha za Serikali.
Frank
ameongeza kuwa ni muhimu uwepo ushirikiano kati ya vyombo vinavyohusika na
kufanya maamuzi na kutekeleza shughuli mbalimbali katika mchakato wa ununuzi wa
umma.
Vyombo
hivyo ni pamoja na mamlaka ya kuidhinisha bajeti, bodi ya zabuni, kitengo cha
ununuzi, idara tumizi, Kamati ya
tathmini ya zabuni, timu ya majadiliano pamoja na kamati ya ukaguzi.
“Ni
muhimu kushirikiana, kila mmoja atimize wajibu na majukumu yake bila
kuingiliana hatua inayopelekea mchakato wa ununuzi kuwa wa tijakatika ofisi
husika.” alisema Frank.
Kwa
upande wake Mkurugenzi wa Idara ya Ununuzi na Ugavi Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bi Cecilia Kasonga amesema mafunzo yanasaidia
kuwaimarisha katika kutekeleza majukumu yao ambapo ni vema mafunzo yatolewe
mara kwa mara ili kurahisisha kazi na kuwapa fursa wajumbe wa bodi kujua taratibu
za ununuzi wa umma hatua itakayosaidia kutoa maamuzi sahihi.
No comments:
Post a Comment