Na
Englibert Kayombo, WAMJW – Dodoma.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewahakikishia
wananchi kuwa Serikali inayo fedha za kutosha kukamilisha ujenzi wa Hospitali
ya Uhuru.
Rais
Magufuli amesema hayo leo alipokuwa akizungumza na wananchi mara baada ya
kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa hospitali hiyo inayojengwa wilayani Chamwino,
Dodoma.
“Fedha
ya ujenzi wa hospitali ipo, tunayo Billioni 3.4” amesema Rais Magufuli ambaye
ameonyesha kutoridhishwa na kasi ya ujenzi wa Hospitali hiyo.
Rais
Magufuli amesema kuwa mwanzoni TBA ilipewa kazi ya ujenzi wa hospitali hiyo lakini
hawakusimamia vizuri ujenzi kupelea Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.
Seleman Jafo kuchukua maamuzi ya kukabidhi kazi kwa Jeshi la Kujenga Taifa ili
kazi hiyo ikamilike kwa wakati.
Naye
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Brigedia Jenarali Charles Mbuge aliyepewa jukumu
la kusimamia ujenzi wa Hospitali hiyo amesema kuwa Jeshi lake linauwezo wa
kufanya kazi hiyo na kuikamilisha ndani ya muda uliopangwa.
“Mheshimiwa
Amiri Jeshi Mkuu, Jeshi letu lina nguvu ya kutosha na tutamaliza kwa muda kazi
hii, sina mipango mingine ni kumaliza tuu” amesema Brigedia Jenerali Mbuge.
Mnamo
tarehe 9 Desemba, 2018, Rais Magufuli alitoa maagizo ya fedha zilizotengwa
kugharamia sherehe za uhuru kiasi cha Shilingi Milioni 995 kutumika kujenga
hospitali katika Mkoa wa Dodoma. Kukamilika kwa hopitali hiyo kutatatua kero
waliyokuwa wanaipata wananchi ya umbali wa kufuata huduma za afya.
No comments:
Post a Comment