Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Kepteni George Mkuchika akikata
utepe kuzindua kampeni ya Utatu itawezekana na Mfumo wa kuripoti matukio ya
rushwa (Takukuru App) uliofanyika katika Viwanja wa Mnazi Mmoja, Jijini Dar es
Salaam.
Na.Mwandishi Wetu.01-11-2019.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utwala Bora,
Kapteni, George Mkuchika amewataka wananchi kuiunga mkono Serikali katika
kupambana na Rushwa ili kupunguza ajali za barabarani pamoja na kuwezesha
upatikanaji wa haki kwa wananchi.
Akizungumza katika uzinduzi wa Kampeni ya kuzuai
rushwa barabarani Waziri Mkuchika amasema kuwa katika kampeni hiyo ijulikanayo
kama “Utatu inayohusisha Taasisi ya kuzuia na Kupambana na Rushwa Takukuru, Jeshi la Polisi na
Wananchi inawezekana na itasaidia katika kutoa taarifa za rushwa zishughulikiwe
kwa haraka ili kupunguza ajali barabarani.
“ Nyote mtakubaliana na mimi kuwa jukumu la kupambana
na rushwa lilikasimiwa kwa Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa Takukuru,
ili kukabiliana na vitendo vya Rushwa vinavypatikana katika maeneo yetu,kila
mmoja wetu anapaswa kubeba jukumu la kupambana kama kampeni hii inavyoeleza”,
alisema Waziri Mkuchika.
Alisema kuwa mara nyingi vitendo vya rushwa
vinafanyika pale ambapo watu wanafanya kazi, wanafanya biashara, wanapata
huduma na kwenye makazi kwa hiyo inawezekana kwa kila mtu kuchukua jukumu la
kuzuia rushwa kwa sababu inatokea kwenye maeneo ambayo wananchi wanahusika,wanaisikia
na kuona vitendo hivyo katika mazingira tofauti.
Waziri Mkuchika alieleza kuwa iwapo kila mtanzania
atachukua dhamira ya dhati ya kuiunga mkono Serikali katika mapambano hayo,
ajali za barabarani zitapungua, kwani mpaka sasa takwimu za mwaka 2018/2019
zinaonesha kuwa ajali za barabara zimepungua kwa kushirikisha wadau, Polisi na
Taasisi ya kupambana na rushwa Takukuru.
Aidha Waziri Mkuchika amezindua Mfumo wa kitekenolojia
unaoitwaTakukuru App unaopatikana kwenye simu ambao utatumika kuripoti vitendo
vya Rushwa katika maeneo mbalimbali nchini.
“Mfumo huu ni mzuri kwani unamuwezesha mwananchi
kukusanya taarifa na matukio ya vitendo vya rushwa kwa kutumia simu ya Mkononi
na kuwasilisha kwa takukuru au jeshi la Polisi
ambapo zitafanyiwa kazi na mtuhumiwa kufikishwa sehemu husika”, Alisema
Waziri Mkuchika.
Kwa upande wake Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, IGP
Simon Sirro amesema kuwa Serikali inatakeleza jukumu kubwa la kuleta usawa wa
haki kwa wananchi nchini kwa kupambana na rushwa ikiwemo ufisadi ili kuleta
maendeleo kwa wananchi, kwa hiyo Jeshi la Polisi linaunga mkono jukumu hilo
ambalo linafanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe
Magufuli.
“ Mchakato wa kampeni hii ni sehemu ya matakwa ya
kihistoria na kitaasisi katika jitihada za kupambana na rushwa nchini
iliyoanzishwa chini ya sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa kifungu namba 11
ya mwaka 20007, sheria hii ilitungwa baada ya kufutwa kwa sheria ya kuzuia
rushwa ya Takukuru sura 329 ambayo ilifanyiwa marejeo mwaka 2002, kwa hiyo
katika kutekeleza majuku haya kampeni hii ambayo mchakato wake ulianza Novemba,
2017 leo inazinduliwa itasaidia sana kupunguza ajali barabarani”, Alisema IGP.
Sirro.
No comments:
Post a Comment