Habari za Punde

Waziri Mhe.Simbachawene Azungumza na Mkurugenzi wa Carbon Tanzania.

Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Taasisi ya Carbobn Tanzania Bw. Mark Barker aliyemtembelea ofisini kwake jijini Dodoma ambapo wamejadili namna ya kusaidia wananchi kuwa na matumizi bora ya ardhi kupitia mradi wa REDD unaotekelezwa na taasisi hiyo katika wilaya ya Mbulu, Tanganyika na Kiteto.
Katika mazungumzo hayo pia Simbachawene aliiomba taasisi hiyo kupeleleka miradi hiyo katika mikoa ya Tabora, Singida na Dodoma ili wananchi wa maeneo hayo wapate elimu hiyo
Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene akiagana na Mkurugenzi wa Taasisi ya Carbobn Tanzania Bw. Mark Barker mara baada ya kufanya nae mazungumzo ofisini kwa waziri.

                                                         Picha na Robert Hokororo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.