Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo
Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe akizungumza na wadau wa michezo wa Jiji la Arusha
alipokua katika ziara ya kujadili maendeleo ya sekta hiyo pamoja na kutatua
changamoto wanazokutana nazo wadau hao iliyofanyika Januari 25,2020.Kulia ni
Katibu tawala Wilaya ya Arusha mjini Bw.Davis Mwaiposa.
Waziri wa Habari
Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe amewaagiza maafisa
michezo wote chini kubadilika katika utendaji wao kutokana na kulalamikiwa na
wadau wengi wa michezo namna ambavyo wanashughulikia sekta hiyo
Waziri Mwakyembe
ametoa agizo hilo jana Jijini Arusha alipokutana na wadau wa michezo kujadili
maendeleo ya sekta hiyo ambapo amewataka maafisa michezo kuhakikisha masuala ya
michezo katika maeneo yao hayakwami kutokana na wao kutowajibika.
“Nyinyi ni watumishi
wa Serikali mnaposhindwa kutatua kero za wanamichezo na kusimamia sekta hii
basi nyie hamtoshi na mimi sitawavumilia kuona mnakwamisha maendeleo ya michezo
nchini”alisema Dkt.Mwakyembe.
Aidha Mhe.Waziri
ameliagiza Baraza la Michezo la Taifa (BMT) ifikapo Februari mosi 2020,liwe limewasilisha
mapendekezo ya mabadilio ya Katiba ya Chama cha Riadha nchini ili kupata
muongozo wa mchezo huo.
Mhe.Waziri ameongeza
kuwa Serikali imerudisha michezo ya UMITASHUMTA na UMISETA ili kuhakikisha
sekta hii inaendelea kukua na kuletea heshima taifa, huku akieleza kuwa
Serikali inadhamiria kutofautisha viwanja vya sanaa na vya michezo kwasabu
sekta hizi zina wadau wengi ambao wamekuwa na matukio yanayofanana na yanayofanyika kwa wakati unaofanana hivyo ni
vyema kila sekta ikajitegema katika maonyesho yake.
Vile vile
Dkt.Mwakyembe amevitaka vilabu vya michezo na mashirikisho kuona umuhimu wa
kutumia wanamichezo wa ndani ili kuinua vipaji walivyonavyo lakini pia
kuwapatia ajira kuliko kusajili wachezaji wa nje wengi na kuwaacha wazalendo.
Kwa upande wake Afisa
Michezo wa Mkoa Bibi Mwamvita Okeng’o amesema
kuwa Mkoa wa Arusha unaendelea kufanya vizuri katika michezo na unaendelea
kukuza sekta hiyo kwa kuongeza idadi ya viwanja na tayari mipango imeanza ya
kujenga uwanja kila Wilaya ya mkoa huo.
Katika hatua nyingine
Makamu Mwenyekiti wa Shirikisho la Riadha Bw.Wiliam Kalaghe amesema kuwa
maandalizi ya wanamichezo Alphonce Simbu na Failuna Abdu ambao wataliwakilisha
Taifa mwaka huu katika mashindano ya Olympiki
huko Japan yanaendelea vizuri na
tayari shirikisho hilo limetoa kiasi cha Sh. Milioni 03 kama chagizo la
maandalizi hivyo watanzania wanapaswa
kuwaunga mkono.
Naye Bw.Hamis mdau wa
mchezo wa mpira wa miguu ameshauri wanamichezo kujifunza lugha na namna bora ya
kufanya mahojiano ili wanapokuwa wamepata nafasi ya kucheza soka nje wasikwame
kwa kigezo cha kushindwa kujibu maswali au kutumia lugha Fulani.
Baadhi ya wadau wa Michezo wa mkoa wa Arusha wakitoa maoni yao wakati wa
kikao cha Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison
Mwakyembe na wadau hao kujadili maendeleo ya sekta hiyo pamoja na kutatua
changamoto wanazokutana nazo iliyofanyika
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo
Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi
wa Mkoa wa Arusha pamoja na wadau wa michezo mkoa huo mara baada ya kumaliza
mkutano wa kujadili maendeleo ya sekta
hiyo pamoja na kutatua changamoto wanazokutana nazo wadau hao uliofanyika
Januari 25,2020.
No comments:
Post a Comment