Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Katibu wa Kamati ya Uhamasishaji na Halaiki Zanzibar,Ndg Ali Mohammed Bakari, alipowasili katika Viwanja vya Polisi Ziwani Jijini Zanzibar kuhudhuria hafla ya Chakula Maalum alichowaandalia Vijana wa Halaiki wakati wa Maadhimisho ya Miaka 56 ya Mapinduzi Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein ameungana pamoja na Vijana wa Halaiki
na wahamasishaji walioshiriki katika
maadhimisho ya sherehe za miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar, katika chakula
maalum alichowaandalia.
Chakula hicho maalum cha mchana aliwaandalia kinatokana na ushiriki wao kwenye sherehe hizo
za miaka 56, zilizofanyika January, 12 mwaka huu katika Uwanja wa Amani,mjini
Unguja.
Hafla hiyo ilifanyika leo
katika Viwanja vya Polisi Ziwani na kuhudhuriwa na Viongozi mbali mbali wa Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar, akiwemo Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idd,
Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu na Naibu Spika wa Baraza la
Wawakilishi Mgeni Hassan Juma.
Wengine ni pamoja na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu
Mkuu Kiongozi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Said
Hassan Said, Mawaziri, Naibu Mawaziri pamoja na Washauri wa Rais wa Zanzibar.
Katika shukrani zake Rais Dk. Shein kwa vijana hao zilizotolewa
kwa niaba yake na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Issa Haji Ussi ‘Gavu’, alisema
ana imani kubwa kuwa vijana hao watakuwa sehemu ya ulinzi wa Taifa hili
kutokana na kujitowa kwao na uzalendo waliouonesha.
Alisema katika kipindi chote cha maandalizi ya sherehe
hizo vijana hao walikuwa wakipokea vyema maelekezo wanayopewa
na Viongozi wao na kuyafanyia kazi kwa
maslahi ya taifa.
Aliwatakiwa kheri na mafanikio katika masomo yao ili waweze
kufaidika katika maisha yao na kulisaidia Taifa kupiga hatua za kimaendeleo.
Aidha, alimpongeza Rais Dk. Shein kwa uongozi wake madhubuti
uliopelekea kuwepo kwa amani na utulivu, umoja na mshikamano, na kusema umesaidia sana kuharakisha maendeleo ya
kiuchumi hapa nchini.
Waziri Gavu aliwashukuru vijana hao kwa kufanikisha vyema
sherehe hizo, huku akitumia fursa hiyo kuwashukuru wananchi wote waliohudhuria
sherehe hizo zilizofana sana.
Nae, Katibu wa Halaiki na Uhamasishaji Ali Mohamed Baraka
alitoa shukurani za dhati kwa Rias Dk. Shein kwa mwaliko huo na kutoa ahadi ya
vijana hao kuendelea kushirikiana na Serikali ili kufanikisha vyema shughuli
zinazoandaliwa.
Aidha, alimshukuru Rais Dk. Shein kwa kuwa karibu na vijana hao
na kuonyesha imani upendo mkubwa kwao.
Hafla hiyo ilipambwa kwa matumbuizo kutoka mashirikiano ya wasanii kutoka fani mbali
mbali, ikiwemo taarabu asilia, Zenj Fleva, Muziki wa Dansi na ngoma za asili.
Abdi Shamna, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax: 024
2231822
E-mail: abdya062@gmail.com
No comments:
Post a Comment