Na. Immaculate Makilika – MAELEZO
Rais Dkt. John Pombe Magufuli amewapa pole wananchi walioathiriwa
na mafuriko yaliyotokea hivi karibuni mkoani Lindi.
Akizungumza jana (Jumatano, Januari 5, 2020) alipokuwa kwenye mkutano wa
hadhara uliofanyika kwenye kijiji cha Kipindimbili, wilaya ya Kilwa mkoani
Lindi, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisema kuwa Rais Magufuli anawapa pole
wananchi waliokumbwa na mafuriko, huku akiwataka wananchi hao kuhama katika
maeneo ya mabondeni.
"Pokeeni
salamu za pole ninazozileta kwenu kutoka kwa Rais wetu mpendwa, Dkt. John
Magufuli alizozitoa kwa wananchi wote mliokumbwa na mafuriko haya kwa kupoteza
ndugu zenu wapendwa pamoja na mali." Alisema Waziri Mkuu
Aidha,
Waziri Mkuu aliwataka Wakuu wa Mikoa na Wilaya nchini kuhakikisha wananchi waliohamishwa
kutoka mabondeni kwenda kwenye maeneo salama hawarejei tena, ili kunusurika na maafa ya mafuriko yanayoweza kujirudia
kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha nchini.
Waziri Mkuu alitembelea vijiji vingine vilivyokumbwa na
maafa hayo ambavyo ni Nambilanje (Ruangwa), Nakiu na Njinjo (Kilwa) na
Kitomanga (Lindi) ili kujionea athari za mafuriko na kuwapa pole wananchi.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa
Lindi, Godfrey Zambi, alisema mvua hizo zilizonyesha mfululizo zilisababisha
maafa makubwa ambapo watu 21 walifariki huku wengine 26,481 katika kaya 4,344
wakikosa makazi.
Vilevile, Mkuu huyo wa Mkoa,
alitaja maeneo yaliyoathiriwa na mvua hizo kuwa ni shule, zahanati, miundombinu
ya barabara na mashamba.
Mkuu huyo wa Mkoa, alisema kuwa
Ofisi yake ilipokea misaada ya vyakula, nguo, dawa na vifaa vya shule kutoka
kwa wadau mbalimbali, pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia Idara ya Mafaa
ambayo imetoa mahema 80, mablanketi 50, ndoo 1,500, mikeka 350 pamoja na
vikombe 350.
No comments:
Post a Comment