Mratibu wa Kitaifa wa Mtandao wa watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), Onesmo Olengurumwa (kulia) akiongea na Mwenyekiti wa THBUB, Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu (kushoto) alipomtembelea ofisini kwake jijini Dodoma leo Februari 24, 2020. Ambapo pamoja na mambo mengine alipongeza uamuzi wa Rais John Magufuli wa kuwateua Makamishna hao wa tume.
Mwenyekiti wa THBUB, Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu (kushoto) akiaga Mratibu wa Kitaifa wa Mtandao wa watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), Onesmo Olengurumwa (kulia) mara baada ya kumaliza kikao chao kifupi kilichofanyika katika ofisi za THBUB leo, Februari 24, 2020.
Na. Mbaraka Kambona,
Mtandao
wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) nchini umepongeza hatua ya Mheshimiwa
Rais John Pombe Magufuli ya kuwateua Makamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na
Utawala Bora (THBUB).
Pongezi
hizo zimetolewa na Mratibu wa Kitaifa wa Mtandao huo, Onesmo Olengurumwa alipokutana na
Mwenyekiti wa THBUB, Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu ofisini kwake jijini Dodoma leo
Februari 24, 2020.
Akiongea
na Mwenyekiti huyo wa THBUB alisema kuwa uteuzi huo umefurahiwa na wadau wengi
wa haki za binadamu kwani utaiwezesha
tume kufanya kazi zake kama inavyopaswa.
Alisema
kuwa THBUB ni chombo cha kitaifa ambacho kimeundwa kikatiba na kupewa mamlaka
ya kuhamasisha na kulinda haki za binadamu nchini na wananchi wengi
wanakitegemea chombo hicho kwa ajili ya kuwasidia kutetea haki zao.
Aliongeza
kwa kusema kuwa THBUB kukaa muda mrefu bila Makamishna kulikwamisha mambo mengi
kwa kuwa wao ndio wenye kufanya maamuzi mbalimbali katika taasisi hiyo.
Olengurumwa
alisema pia kukosekana kwa Makamishna hao kulipelekea kudorora kwa ushirikiano
baina ya wadau wa haki za binadamu na taasisi hiyo, lakini sasa anaamini kwa
kuwepo wao katika uongozi huduma za tume kwa wananchi zitatolewa kama
inavyotegemewa.
Aidha,
Olengurumwa alimuhakikishia Mwenyekiti wa THBUB ushirikiano wa karibu na kumueleza kuwa watakaa kuona maeneo gani
wanaweza kushirikiana, lakini kwa kuanzia alimuahidi Jaji Mwaimu kuwa THRDC
itatoa mafunzo ya kuwajengea uwezo maafisa wa tume kuhusu namna bora ya kufanya utetezi wa haki za binadamu kwa
wananchi.
Akiongea
mapema wakati akimkaribisha Mratibu huyo, Jaji Mwaimu alimueleza kwa ufupi
kuhusu majukumu ya THBUB na mipango ya
taasisi hiyo kwa mwaka huu.
Aidha
mwenyekiti huyo aliahidi kuendelea kushirikiana na wadau wote wakiwemo THRDC
akisema kuwa tume peke yake bila kushirikiana na wadau wengine haitaweza
kutimiza majukumu yake ipasavyo.
Rais
John Magufuli alifanya uteuzi wa Makamishna hao mwishoni mwa mwaka jana baada
ya THBUB kukaa bila Makamishna kwa takriban miaka mitatu.
MAELEZO
YA PICHA
PICHA
NAMBA 6222
Mratibu
wa Kitaifa wa Mtandao wa watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), Onesmo
Olengurumwa (kulia) akiongea na Mwenyekiti wa THBUB, Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu
(kushoto) alipomtembelea ofisini kwake jijini Dodoma leo Februari 24, 2020.
Ambapo pamoja na mambo mengine alipongeza uamuzi wa Rais John Magufuli wa
kuwateua Makamishna hao wa tume.
PICHA
NAMBA 6248
Mwenyekiti
wa THBUB, Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu (kushoto) akimuaga Mratibu wa Kitaifa wa
Mtandao wa watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), Onesmo Olengurumwa (kulia)
mara baada ya kumaliza kikao chao kifupi kilichofanyika katika ofisi za THBUB
leo, Februari 24, 2020.
No comments:
Post a Comment