Balozi wa hiari wa Utalii wa Tanzania nchini
Uingereza, Bw.Nick Reynald ‘Bongozozo’ akifafanua jambo kwa Waandishi wa Habari
(hawapo pichani), katika hafla fupi ya kupewa Ubalozi wa Utalii wa Tanzania
nchini Uingereza iliyofanyika Jijini Dar es Salaam, leo Februari 04, 2020,
kulia ni Afisa Uhisiano Mkuu TTB, Geofrey Tengeneza na kushoto ni Meneja Masoko
kutoka Bodi ya Utalii (TTB), Geofrey Meena.
Meneja Masoko kutoka Bodi ya Utalii (TTB), Geofrey
Meena akifafanua jambo kwa Waandishi wa Habari (hawapo pichani), katika hafla
fupi ya kupewa Ubalozi wa Utalii wa Tanzania nchini Uingereza kwa bwana Nick
Reynald ‘Bongozozo’ iliyofanyika Jijini Dar es Salaam, leo Februari 04, 2020,
kulia ni Afisa Uhisiano Mkuu TTB, Geofrey Tengeneza na kushoto ni Balozi wa
hiari wa Utalii wa Tanzania nchini Uingereza, Bw.Nick Reynald ‘Bongozozo’
Meneja Masoko kutoka Bodi
ya Utalii (TTB), Geofrey Meena(kushoto) akimkabidhi jarida la utalii (Tanzania
Unforgetable)Bw. Nick Reynald ‘Bongozozo’(katikati) aliyekabishiwa barua rasmi kuwa balozi wa
hiari wa utalii wa Tanzania nchini Uingereza, kulia ni Afisa Uhisiano Mkuu TTB, Geofrey
Tengeneza
Meneja Masoko kutoka Bodi ya Utalii (TTB), Geofrey
Meena(kushoto) akimkabidhi FLASH yenye
video za utalii wa Tanzania balozi wa
hiari wa utalii wa Tanzania Bw.Nick
Reynald ‘Bongozozo’(katikati)
aliyekabishiwa barua rasmi leo Februari 04,2020, kulia ni Afisa Uhisiano
Mkuu TTB, Geofrey Tengeneza.
Meneja Masoko kutoka Bodi ya Utalii (TTB), Geofrey
Meena(kushoto) akimkabidhi jarida la utalii (SiTE) Bw.Nick Reynald
‘Bongozozo’(katikati) aliyekabishiwa
barua rasmi kuwa balozi wa hiari wa utalii wa Tanzania nchini Uingereza, kulia ni Afisa Uhisiano Mkuu TTB, Geofrey
Tengeneza
Picha na Idara ya Habari-MAELEZO
Na. Mwandishi Wetu-MAELEZO
Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Bodi ya Utalii
nchini (TTB), leo imetekeleza agizo la Waziri wa Wizara hiyo, Dkt.Hamisi Kingwala
alilolitoa Jijini Dodoma jana Februari 03,2020 la kumpa Mwingireza Nick Reynald
maarufu kama Bongozozo ubalozi wa utalii wa Tanzania nchini Uingireza.
Akizungumza katika hafla ya kumkabidhi barua ya
utambuzi kwa ajili ya kazi hiyo iliyofanyika Jijini Dar es Salaam, Meneja
Masoko wa TTB, Geofrey Meena alisema kuwa, Nick Reynald aliyezaliwa Zimbabwe na
kuishi Tanzania kwa miaka 18 yaani tangia mwaka 1998 atakuwa balozi mzuri kwa
uitalii wa Tanzania kwa sababu maeneo mengi ya utalii anayajua.
“Nick Reynald ‘Bongozozo’ ameishi hapa nchini kwa
miaka mingi kuanzia mwaka 1998 mpaka sasa ni miaka 18 kwa hiyo anauelewa na
utalii wa Tanzania, amekuwa maarufu sana hapa nchini kutokana na mapenzi makubwa kwa Tanzania ambayo yemejidhihirisha
katika nyanja nyingi ikiwemo ushabiki wa mpira kwa timu ya Taifa ‘Taifa Stars”
pamoja na wachezaji akiwemo Mbwana Samatta anayekipiga kunako klabu ya mpira ya
Astoni villa nchini Uingireza”, Alisema Geofrey Meena.
Meena alisema kuwa Bongozozo alivutiwa sana na soka la
Tanzania kwa kuwa kuna fujo isiyoumiza na amekuwa akisafiri na Timu ya Taifa
‘Taifa Stars’ katika michuano mbalimbali ikiwemo ile ya AFCON ambayo kwa mwaka
2019 ilifanyika nchini Misri.
TTB imedhamiria kukuza utalii kwa kuongeza watalii
kutoka Uingereza kwa kuwa nchi hiyo ni ya pili kwa kuleta watalii wengi nchini
ikitanguliwa na Marekani, kwa takwimu za utalii mwaka 2018, watalii kutoka
Uingereza walikuwa 77,199 huku Marekani ikileta watalii 94,876.
“Bodi inayofuraha leo kwa niaba ya Waziri mwenye
dhamana ya Utalii nchini, kumkabidhi rasmi Nick Reynald ‘Bongozozo’ barua ya
uteuzi wa kuwa balozi wa Hiari wa utalii
wa Tanzania nchini Uingereza kama kituo bora cha utalii Afrika na duniani
kote”, Alisema Geofrey Meena.
Kwa upande wake Nick Reynald ‘Bongozozo ambaye kwa sasa ni Balozi wa utalii wa
Tanzania nchini Uingereza alisema kuwa yeye atakuwa balozi mzuri katika
kutangaza mazuri ya Tanzania na utalii wake duniani kote kupitia mitandao yake
ya kijamii ili kuleta watalii nchini.
“Nikizunguka duniani kote kupitia mitandao yangu ya
kijamii nitawaambia kuwa Tanzania ni nchi yenye watu wakarimu sana, nitazidi
kuipeperusha bendera ya Tanzania na nitawaeleza sehemu za kitalii zilizoko
Tanzania, kwahiyo nimekubali kuitangaza Tanzania kwa watalii wengi duniani”,
Alisema Nick Reynald ‘Bongozozo.
No comments:
Post a Comment