Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akiongea na
washiriki wa Bonanza la kuibua vipaji vya uimbaji lililofanyika mwishoni mwa
wiki wilayani Same mkoa wa Kilimanjaro lililoongozwa na kaulimbiu “Tutambue
vipaji vyetu tujiajiri kufikia uchumi wa kati na JPM.”
Na
Eleuteri Mangi, WHUSM-Same
Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe ameagiza Baraza
la Sanaa la Taifa (BASATA), Bodi ya Filamu pamoja na Kamati ya Maudhui ya Mamlaka
ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) wafanye kazi yao ya kisheria ya kulinda maadili
ya jamii ya Kitanzania ili taifa liendelee kufuata misingi imarya utamaduni na
sanaa iliyoasisiwa na viongozi wetu.
Dkt.
Mwakyembe ametoa agizo hilo wakati wa mashindano ya Bonanza ya kuibua vipaji
vya uimbaji lililofanyika mwishoni mwa wiki wilayani Same mkoa wa Kilimanjaro
ambalo liliongozwa na kaulimbiu “Tutambue vipaji vyetu tujiajiri kufikia uchumi
wa kati na JPM.”
Akizunumzia
umhimu wa sanaa na utamaduni katika jamii
Waziri amesema “Huwezi kuruhusu upuuzi huu unaendele wa kuharibu watoto wetu
kabla hawajakua, haiwezekani kuanza kurusha vipindi vya ajabu ajabu asubuhi,
tuna sheria tumepitisha Bungeni ipo wazi.
Nyimbo zote zenye mashaka mashaka
ambazo inabidi waangalie watu wazima zianze kupigwa kuanzia saa 6:00 usiku, ipo
kwenye sheria situngi mimi sasa hivi na mwisho ni saa 11:00 alfajiri,
tusijiachie hivi Watanzania, haiwezekani” alisisitiza Dkt. Mwakyembe.
Waziri
huyo mwenye dhamana ya sekta ya habari, amevitaka vyombo vya habari kwa washirikiane
na BASATA, Bodi ya Filamu pamoja na Kamati ya Maudhui ya TCRA kutekeleza agizo
hilo kwa kuzingatia ukweli kuwa kuna taifa ambalo lina wajibu wa kutekeleza na
kuendeleza maadili ya nchi na hatua itakayosaidia kuwaendeleza na kutokuharibu watoto
wadogo kwa kutekeleleza wajibu wa taasisi hizo wa kisheria.
“Naviagiza
vyombo hiyo, hebu fanyeni kazi yenu, jamani tuwape watoto haki yao ili wakue
kama sisi tulivyokuwa, haiwezekani mtoto mdogo wa miaka mitatu amekomaa ukimwangalia
machoni amekomaa kwa ajili ya kuonyeshwa vitu vya ajabu ajabu vya kijinga.
Nalisema
hili sio kwa mzaha, kuanzia Machi 1, 2020 nikiona vyombo vyetu vya televisheni
na redio maudhui yao yanakiuka maadili yetu halafu vyombo vyetu vinavyosimamia
maadili vimekaa kimya, heri tuwabadilishe tuweke watu wapya waweze kufanya kazi
ya kulinda maadili ya mtanzania” alisema Dkt. Mwakyembe
Aidha,
Waziri amesisitiza kufurahishwa na washiriki wa Bonanza hilo la kuibua vipaji
Same ambapo vikundi na washiriki wote wameonesha wananidhamu kwa kuzingatia maadili
ya mtanzania ambayo wameyalinda, yanaendelezwa na kuwafanya waimbe vizuri wakiwa
wamevaa mavazi ya heshima kulingana na maadili ya kitanzania.
Kwa
upande wake Mkuu wa wilaya ya Same Rosemary Senyamule amesema washindi wa bonanza
hilo watapata fursa ya kurekodi kazi zao ambazo zitatumika katika vyombo vya
habari ndani na nje ya nchi ambazo zitasaidia kuhabarisha, kuelimisha na
kuburudisha jamii.
Pia
amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa
dhamira ya dhati aliyoionyesha katika kuinua wasanii kwa kutoa Shilingi milioni
100 mwaka 2019 kwa ajili ya kusaidia kazi za sanaa na amekuwa mfano wa kuigwa
kila eneo ambapo na wao kama wasaidizi
wa Rais wanaunga mkono katika maeneo yao ikiwemo Bonanza la kuibua vipaji
wilayani Same.
Aidha,
amesema kuwa Dkt. Mwakyembe amekuwa msatari wa mbele katika kutatua changamoto
za wasanii ikiwemo maboresho ya Sheria zinazopelekea kulinda haki wasanii hatua
inayowatia wasanii moyo kwa kutambua juhudi za Serikali katika kazi zao za
sanaa.
Naye
Balozi wa Utalii na Mdau wa Maendeleo
Tanzania Nangasu Werema amesema anaipenda nchi yake Tanzania na
maendeleo yanayoletwa na Serikali ya Awamu ya Tano na kuwahamasisha watanzania
kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi ambapo kuna mradi endelevu wa
kuhakikisha wanayama aina faru unaendelezwa na hatimaye kuchangia pato la taifa
na hivyo kukuza uchumi wa nchi ambao unatajiwa kuifikisha Tanzania katika
uchumi wa kati ifikapo 2025.
Bonanza
la kuibua vipaji vya uimbaji wilayani Same mwaka huu linafanyika kwa mara ya pili
tangu kuanza kufanyika mwaka 2019 ambapo limekuwa na mafaniko mengi ikiwemo
mwitikio wa wananchi wengi kushiriki bonanza hilo katika fani za nyimbo
mbalimbali ikiwemo kwaya, bongo fleva, ushairi pamoja na ngoma za asili ambazo zilitafsiriwa
katika maudhui ya Uchaguzi Mkuu wa 2020, Mafannikio ya Serikali ya Awamu ya
Tano pamoja na Utunzaji wa mazingira na kuendeleza utalii nchini.
No comments:
Post a Comment