Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara ya
Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bw.Petro Lyatuu akizungumza katika kikao cha
kujadili maeneo ya ushirikiano baina ya Serikali ya SMT na SMZ.Kulia ni
Mwenyekiti wa kikao hicho Bw Mahmoud Omar Hamad ambaye ni Mkurugenzi wa
Mipango,Sera na Utafiti kutoka Wizara ya Habari,Utalii na mambo kale Zanzibar.
Kikao hicho kilichofanyika Machi 02,2020 Mjini Zanzibar.
Na Shamimu Nyaki – WHUSM,Zanzibar
Katika kuimarisha Muungano Serikali ya Tanzania
Bara na Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar katika Sekta za Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo zimeendelea kutekeleza vizuri maeneo ya ushirikiano ambayo
yameridhiwa na pande hizo.
Hayo yamebainika leo visiwani Zanzibar katika
Kikao cha Wataalam wa Sekta hizo kutoka pande mbili za serikali wakati
walipokuwa wakijadili utekelezaji wa maazimio yaliyoridhiwa na Mawaziri
wanaosimamia sekta hizo mwezi julai 2019 ambapo Shirika la Utangazaji Tanzania
(TBC) pamoja na Shirika la Utangazaji Zanzibar(ZBC) yameendelea kushirikiana
katika kuhabarisha umma kwa wakati na kwa usahihi shughuli zote zinazotekelezwa
na Serikali ikiwemo Miradi ya Maendeleo pamoja na kubadilishana utaalamu katika
sekta hiyo.
Akizungumza katika kikao hicho Mwenyekiti
Bw.Mahmoud Omar Hamad ambaye ni Mkurugenzi wa Mipango,Sera na Utafiti wa Wizara
ya Habari,Utalii na Mambo kale amesema kuwa lengo la kikao hicho ni kupitia
taarifa ya utekelezaji iliyotokana na kikao cha mawaziri kilichofanyika julai
2,Jijini Dodoma kilichoelekeza kuimarisha maeneo ya ushirikiano baina ya
serikali zote mbili ambayo yana tija katika Muungano.
“Kikao hichi kina lengo la kutafuta suluhisho katika
maeneo ambayo yana changamoto katika ushirikiano wetu lakini pia kuibua maeneo
mapya ya ushirikiano ambayo yatakuwa na faida kwa pande zote mbili za muungano
wetu”alisema Bw.Mahmoud Omari.
Katika maeneo ambayo Serikali hizo zinashirikiana
katika sekta ya habari zimefanikiwa kuwapatia maafisa habari ufadhili wa masomo
katika ngazi ya Shahada ya Uzamili nchini China ambapo maafisa mawili kutoka
SMT na SMZ walipata nafasi hiyo na sasa wapo masomoni.
Vilevile katika Sekta ya Utamaduni Baraza la
Kiswahili la taifa (BAKITA) pamoja na Baraza la Kiswahili Zanzibar (BAKIZA)
zimafanikiwa kuandaa Kanzidata ya kusajili wataalamu wa lugha ya kiswahili
ngazi ya shahada ya kwanza,Uzamili na Uzamivu ambapo hadi sasa jumla ya waalimu
wa kufundisha Kiswahili 1,224 kutoka SMT na 414 kutoka SMZ wamesajiliwa.
Hata hivyo katika Sekta ya Michezo ushirikiano
umeendelea kuwepo kwa kuwa WHUSM,OR TAMISEM na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia
zimekua zikiendesha mashindano ya michezo shuleni ya UMISSETA na
UMITASHUMTA ambapo kwa upande wa
Zanzibar michezo ya UMISSETA ndio inayoshiriki na tayari Serikali zote mbili zimekubaliana
kuanzisha mashindano ya UMITASHUMTA visiwani humo.
Kikao hicho ni cha awali ambacho kitafuatiwa na
kikao cha Makatibu Wakuu na baadae kufuatiwa na kikao cha Mawaziri wanaosimamia
sekta hizo.
Mwenyekiti wa kikao cha kujadili maeneo ya
ushirikiano baina ya Serikali ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) Bw Mahmoud Omar Hamad ambaye ni Mkurugenzi wa
Mipango,Sera na Utafiti kutoka Wizara ya Habari,Utalii na mambo kale Zanzibar. Kikao
hicho kilichofanyika Machi 02,2020 Mjini Zanzibar.
Mwakilishi kutoka Kampuni ya magazet ya Serikali
akitoa maoni katika kikao cha kujadili maeneo ya ushirikiano baina ya Serikali
ya Serikali ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
(SMZ).Kulia ni Mkurugenzi msaidizi Idara ya Habari -Maelezo SMT.
Baadhi ya washiriki wa kikao cha kujadili maeneo
ya ushirikiano baina ya Serikali ya Serikali ya Muungano wa Tanzania (SMT) na
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ).Kulia ni Mkurugenzi msaidizi Idara ya
Habari Maelezo SMT.
No comments:
Post a Comment