Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George
Simbachawene (katikati), akizungumza na Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya
Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Victor Mwambalaswa wakati wakitoka
kukagua Jengo la Makao makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, jijini Dodoma
leo. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Ramadhani Kailima. Kamati ya
Bunge imeridhishwa na ujenzi wa Jengo hilo ambalo lipo hatua ya mwisho
kukamilika.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George
Simbachawene (katikati), akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (hawapo pichani), katika kikao cha Kamati hiyo,
kilichofanyika Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, jijini Dodoma, leo.
Kamti hiyo pia ilikagua ujenzi wa Jengo la Makao Makuu ya Jeshi hilo na
imeridhishwa na ujenzi wa Jengo hilo ambalo lipo hatua ya mwisho kukamilika.
Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Ramadhani Kailima, na kulia ni Kamishna Jenerali
wa Jeshi hilo, John Masunga
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George
Simbachawene (kushoto), akiwa na Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo
ya Nje, Ulinzi na Usalama, Almas Maige, wakiliangalia Jengo la Makao Makuu ya
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wakati Kamati hiyo inafanya ukaguzi wa jengo hilo
ambalo lipo hatua ya mwisho kukamilika. Kamati hiyo imeridhishwa na ujenzi wa
jengo hilo
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George
Simbachawene, akiwaonyesha wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya
Nje, Ulinzi na Usalama, uimara wa kuta za jengo la Makao Makuu ya Jeshi la
Zimamoto na Uokoaji, jijini Dodoma, wakati wajumbe hao walipokuwa wanalikagua
jengo hilo ambalo lipo hatua ya mwisho kukamilika. Kamati hiyo imeridhishwa na
ujenzi wa jengo hilo. Wapili kushoto ni Kaimu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Victor
Mwambalaswa.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George
Simbachawene (watatu kushoto-waliokaa), Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya
Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Victor Mwambalaswa
(katikati-waliokaa), Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Ramadhani Kailima
(wapili kushoto-waliokaa), Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,
John Masunga (kulia waliokaa), wakiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa
Kamati hiyo, baada ya kumaliza kufanya kikao na baadaye kulikagua Jengo la
Jeshi hilo, jijini Dodoma,
Muonekano wa Jengo la Makao Makuu ya Jeshi la
Zimamoto na Uoakoji, jijini Dodoma, lipo hatua ya mwisho kukamilika, ambapo
wajumbe wa kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama
walilikagua na kuridhishwa na ubora wa Jengo hilo.
No comments:
Post a Comment