Habari za Punde

WAZIRI SIMBACHAWENE AWAONGOZA WATENDAJI WAKUU ZIMAMOTO KIKAO CHA KAMATI YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA, WAJUMBE WAKAGUA, WARIDHISHWA NA UJENZI MAKAO MAKUU WA JESHI HILO, JIJINI DODOMA

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (katikati), akizungumza na Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Victor Mwambalaswa wakati wakitoka kukagua Jengo la Makao makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, jijini Dodoma leo. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Ramadhani Kailima. Kamati ya Bunge imeridhishwa na ujenzi wa Jengo hilo ambalo lipo hatua ya mwisho kukamilika. 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (katikati), akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (hawapo pichani), katika kikao cha Kamati hiyo, kilichofanyika Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, jijini Dodoma, leo. Kamti hiyo pia ilikagua ujenzi wa Jengo la Makao Makuu ya Jeshi hilo na imeridhishwa na ujenzi wa Jengo hilo ambalo lipo hatua ya mwisho kukamilika. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Ramadhani Kailima, na kulia ni Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo, John Masunga
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (kushoto), akiwa na Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Almas Maige, wakiliangalia Jengo la Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wakati Kamati hiyo inafanya ukaguzi wa jengo hilo ambalo lipo hatua ya mwisho kukamilika. Kamati hiyo imeridhishwa na ujenzi wa jengo hilo
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene, akiwaonyesha wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, uimara wa kuta za jengo la Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, jijini Dodoma, wakati wajumbe hao walipokuwa wanalikagua jengo hilo ambalo lipo hatua ya mwisho kukamilika. Kamati hiyo imeridhishwa na ujenzi wa jengo hilo. Wapili kushoto ni Kaimu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Victor Mwambalaswa. 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (watatu kushoto-waliokaa), Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Victor Mwambalaswa (katikati-waliokaa), Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Ramadhani Kailima (wapili kushoto-waliokaa), Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, John Masunga (kulia waliokaa), wakiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Kamati hiyo, baada ya kumaliza kufanya kikao na baadaye kulikagua Jengo la Jeshi hilo, jijini Dodoma,
Muonekano wa Jengo la Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uoakoji, jijini Dodoma, lipo hatua ya mwisho kukamilika, ambapo wajumbe wa kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama walilikagua na kuridhishwa na ubora wa Jengo hilo. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.