Muonekano wa barabara mpya iliyojengwa kwa kiwango cha katika Manispa ya Kigoma Ujiji kama inavyooneka picha wananchi wakiwa katika harakati zao.
Muonekano wa moja ya
barabara za Manispaa ya Kigoma Ujiji baada ya kujengwa kwa kiwango cha lami
kama ilivyokutwa nyakati za usiku Machi 29, 2020.
Mzunguko wa barabara
eneo laMwanga Sokoni Manispaa ya Kigoma
Ujiji kama ulivyokutwa baada ya kuimarishwa kwa miundombinu ya barabara katika
Manispaa hiyo ikiwemo kuwekwa kwa taa za barabarani, maeneo ya waenda kwa miguu
na ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilomita 12 kwa kiwango cha lami.
Na Frank
Mvungi- MAELEZO Kigoma
Shilingi Bilioni
18.62 zilivyowezesha mageuzi ya
miundombinu ya barabara za lami katika Manispaa ya Kigoma Ujiji .
Akizungumzia
utekelezaji wa mradi huo, Mhandisi wa Manispaa hiyo Injinia Wilfred Shimba amesema kuwa barabara zilizojengwa zina urefu
wa Kilomita 12 na ujenzi huo umehusisha
njia za waenda kwa miguu, mifereji ya maji na taa za barabarani.
“ Awali Manispaa ya
Kigoma Ujiji ilikuwa na barabara moja tu yenye lami na kwa sasa kujengwa kwa
barabara hizi kunachangia kukuza shughuli za kiuchumi na hivyo hata mapato
yanaongezeka na mandhari ya mji inavutia zaidi kwa sasa”, Alisisitiza Mhandisi
Shimba
Akifafanua Mhandisi
Shimba amesema kuwa mradi wa ujenzi wa barabara za Manispaa hiyo umekuwa chachu
ya maendeleo katika Manispaa hiyo na imevutia
na kuchangia kuongezeka kwa shughuli za kiuchumi kwa wananchi.
Alizitaja faida za
mradi huo kuwa ni pamoja na; kurahisisha usafiri na usafirishaji ndani ya
Manispaa hiyo, kuvutia uwekezaji, kufanya Manispaa hiyo kuwa na muonekano bora
zaidi ya ilivyokuwa awali kabla ya kuboreshwa kwa miundombinu hiyo ikiwemo
kuwekwa kwa taa za kuongozea magari.
Akizungumzia
utekelezaji wa mradi huo umekamilika na kuanza kuleta manufaa kwa wakazi wa
Kigoma na wawekezaji wote wanaofika katika Manispaa hiyo kwa lengo la kufanya
uwekezaji katika sekta mbalimbali ili kuchangia katika kukuza uchumi na ustawi
wa wananchi.
Kwa sasa baada ya
kukamilika kwa kazi zote ambazo zipo katika mkataba wa ujenzi wa barabara ikiwa
ni pamoja na ujenzi wa mifereji ya maji ya mvua, imeleta tija katika sehemu
zote za maeneo ya mradi, hususani mfereji wa maji yam vu wa Katonyanga na
barabara zote ili kupunguza adha za maji ya mvua kwa wakazi wa maeneo yote ya
Manispaa ya Kigoma.
Kwa upande wake mkazi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji
Bw. Yasin Ally amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imefanya mageuzi
kwa makubwa katika ujenzi wa miundombinu ya Manispaa hiyo zikiwemo barabara za
lami, taa na huduma za jamii zimeimarishwa.
Aliongeza kuwa kuimarishwa kwa miundombinu ni chachu ya
maendeleo kwa wananchi wa mkoa huo kwa ujumla.
Ujenzi wa barabara za
lami katika Manispaa ya Kigoma Ujiji umefanyika katika mitaa ya Kaaya hadi
Simu, Mwanga Kitabwe Mwembetogwa, Wafipa
Kagera, Kagashe Road, Kukolwa Road, Ujenzi
Nazareth, Maweni Burega.
No comments:
Post a Comment