Afisa
Mfawidhi wa Ofisi za THBUB Kanda ya Ziwa, Albert Kakengi (kushoto) akimuonesha
Kaimu Katibu Mtendaji wa THBUB, Hajjat Fatuma Muya (Kulia) baadhi ya machapisho
kuhusu haki za watoto yaliyopo katika maktaba ndogo ofisini hapo. Wa pili kulia
ni Kaimu Mkuu wa Kitengo Mipango wa THBUB, Laurent Burilo. Uongozi wa THBUB
ulitembelea Ofisi hizo za Mwanza Aprili 20, 2020.
Mwenyekiti
wa THBUB, Jaji (Mst.) Mathew Mwaimu (katikati) akiongea wakati alipomtembelea
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella (kulia) ofisi kwake jijini Mwanza Aprili 20, 2020. Kushoto ni
Kaimu Katibu Mtendaji wa THBUB, Hajjat Fatma Muya.
Mwenyekiti
wa THBUB, Jaji (Mst.) Mathew Mwaimu (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na
Watumishi wa THBUB Kanda ya Mwanza alipoitembelea Ofisi hiyo Aprili 20, 2020. Wapili
kutoka kulia ni Kaimu Katibu Mtendaji wa THBUB, Hajjat Fatuma Muya.
Na
Mbaraka Kambona,
Mkuu
wa Mkoa wa Mwanza, Mh. John Mongella ameishauri Tume ya Haki za Binadamu na
Utawala Bora (THBUB) kuandaa mpango maalamu wa kutoa elimu ya haki za binadamu
na misingi ya utawala bora kwa Watendaji
wa ngazi za mikoa ili waweze kutoa haki za
wananchi kwa wakati.
Mongella
alitoa rai hiyo katika kikao kifupi kilichofanyika baina yake na Mwenyekiti wa
THBUB, Jaji (Mst.) Mathew Mwaimu alipomtembelea ofisini kwake jijini Mwanza Aprili 20, 2020.
Akiongea
katika kikao hicho Mongella alisema kuwa kuna haja Tume kuweka utaratibu wa kutoa
elimu kwa viongozi wa ngazi za mikoa kupitia vikao vyao vya kiutendaji ili
kuwajengea uwezo kuhusu masuala ya haki za binadamu na utawala bora na kujua wajibu wao.
“Ni
vizuri mkaweka utaratibu kupitia vikao vya Watendaji Wakuu katika mikoa ili
kuwaelimisha juu ya dhana nzima ya utoaji
haki kwa wananchi, ni muhimu kuwaelimisha viongozi hawa kujua haki na wajibu
wao, kwani bila kufanya hivyo matatizo
hayo ya kutopata ushirikiano kutoka kwao yataendelea kuwa changamoto kwenu”,
alisema Mongella.
Aliongeza
kuwa taasisi za serikali hazina budi kufanya kazi kwa pamoja kwa sababu lengo
lao ni kuhudumia wananchi, hivyo ni muhimu kupitia vikao hivyo vya watendaji
Tume ikavitumia kuwaelimisha pia kujenga uhusiano utakao warahisishia utendaji kazi
wake.
“Kuna wakati haki inachelewa kushughulikiwa na
viongozi aidha kwa sababu ya uzembe au kwa kiongozi kutokujua wajibu wake katika kutoa haki hiyo ya
mwananchi kwa wakati”, aliongeza Mongella
“Tunaweza
tukawa tunapambana na matokeo wakati kabla ya matokea kuna chanzo. Tutoe elimu
kwa viongozi, tukiweza kuwaelimisha vizuri naamini tutapunguza kushughulika na
matokeo na malalamiko yatapungua”, alisisitiza
Akiongea
mapema, Jaji Mwaimu alimueleza Mkuu wa Mkoa huyo kuwa nia ya Tume ni kuisaidia
na kuijenga zaidi Serikali ili iweze kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi kwa
kuzingatia haki za binadamu na utwala bora na njia pekee ya kufanya hivyo ni
kwa Tume kushirikiana kwa karibu na taasisi nyingine za Serikali ambazo zinatoa
huduma kwa wananchi.
Jaji
Mwaimu aliendelea kusema kuwa ni vigumu kuhamasisha masuala ya haki za binadamu
bila kuwahusisha wadau ambao kwa kiasi kikubwa ni Serikali.
Jaji
Mwaimu alikutana na Mongella ikiwa ni sehemu ya ziara yake jijini Mwanza ambayo
lengo lake kubwa ni kutembelea ofisi za Tume zilizopo kanda ya Ziwa ili
kushughulikia malalamiko ya wananchi yaliyowasilishwa katika ofisi hizo.
No comments:
Post a Comment