Habari za Punde

Uongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoani Iringa Wakabidhi Msaada Kwa Wananchi Waliopata Mafuriko Pawaga.

Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi wilaya ya Iringa Constatine Kihwele akikabidhi msaada huo kwa wananchi wa kitongoji cha Mbingama waliokumbwa na mafuriko kutokana na mvua nyingi za msimu huu.
 
NA FREDY MGUNDA,IRINGA
CHAMA cha mapinduzi wilaya ya Iringa imetoa msaada wa chakula,Nguo na sabuni kwa wahanga wa kuziwezesha kaya zilizokumbwa na mafuriko katika kitongoji cha Mbingama kijijini Isele, tarafa ya Pawaga wilayani Iringa kukabiliana na changamoto ya ambazo nwanakabilia.

Msaada huo unaohusisha unga na maharage ulikabidhiwa kwa mwenyekiti wa kijiji cha Isele kwa niaba ya wahanga hao wa mafuriko katika kitongoji cha Mbingama.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huu mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi wilaya ya Iringa Constatine Kihwele alisema mafuriko yaliyotokea hivikaribuni katika kitongoji hicho yamesebabisha kaya 218 zenye jumla ya watu 801 kuachwa bila makazi huku akiba yao ya vyakula, fedha, nguo na vifaa vyao vingine vikisombwa baada ya nyumba zao kubomoka.

Kihwele alisema kuwa chama cha mapinduzi,serikali na wadau wengine wataendelea kutafuta msaada wa kuwasaidia kutokana na kukumbwa na mafuriko ambayo hawakutarajia.

Aliwataka wadau mbalimbali kuendelea kutoa msaada kwa wahanga hao wa mafuriko kwa kuwa bado wanamahitaji mengi ambayo wanatakiwa kusaidiwa kutokana na kupoteza asilimia kubwa ya mali zao ambazo walikuwa wanamiliki kabla ya kukumbwa na mafuriko hayo.

Kihwele aliwataka wananchi wa kitongoji hicho kilichokumbwa na mafuriko kuendelea kujikinga na ugonjwa wa Corona licha ya kuwa bado wapo katika kipindi kigumu kutokana na mafuriko yaliyowapata.

Naye mwenyekiti wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi wilaya ya Iringa Makalah Mapesa aliwataka wahanga hao wa mafuriko kuanza kutafuta njia ya kujitegemea kwa kuwa msaada huu itafika mahala utaisha na hakutakuwa na mtu wa kusaidia tena.

“Naomba muanze kujifunza kujitegemea kwa kuwa hii misaada tunayoileta hizi saizi inamwisho wake ni bora kuanza kutafuta njia mbadala ya kuanza kuishi maisha yenu ya kawaida kama ambavyo mlikuwa mnaishi hapo awali” alisisitiza Mapesa 

Mapesa alisema kuwa hakuna watu ambao watapewa msaada wa maisha kutokana na kukumbwa na mafuriko hivyo ni bora mkautumia vizuri msaada ambao mnapewa na wadau mbalimbali.

Katika msafara wa kwenda kutoa msaada huo waliambatana na madiwani wanawake wa chama cha mapinduzi wilaya ya Iringa pamoja na katibu wa mbunge wa jimbo hilo Thom Lukuvi

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.