Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na
Mazingira) Mhe. Mussa Sima akiangalia mojawapo ya mawe yanayotumika
kutengenezea chokaa katika kiwanda cha Neelkanth cha jijini Tanga ambacho
kinalalamikiwa na wakazi wa eneo hilo kufikiwa na vumbi.
Na.robert hokororo
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na
Mazingira) Mhe. Mussa Sima amemuelekeza mwekezaji wa kiwanda cha chokaa cha
Neelkanth Chemical cha jijini Tanga kubuni njia mbadala ya kuzuia vumbi kutoka
na kusambaa hewani hivyo kuleta athari kwa wananchi.
Mhe.Sima alitoa agizo hilo jana alipofanya ziara ya kukagua
kiwanda hicho ambapo pamoja na mambo mengine ililenga kumpa maelekezo ya namna
ya kuendesha shughuli bila kuathiri mazingira.
Alibainisha kuwa mashine zilizopo hapo hazina uwezo wa
kuzuia vumbi kusambaa jambo ambalo ni hatari kwa afya ya wafanyakazi na
wananchi wakati moshi unapofuka hewani.
Alilielekeza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa
Mazingira (NEMC) wapime na waangalie ni madhara gani ya kiafya kwani unakwenda
kwenye makazi ya watu.
“Mazingira ya kiwandani hapa ni ya kawaida lakini
tunashuhudia moshi na vumbi vikisambaa ni sawa wana consultant (mshauri) hapa standards (viwango) zinatofautiana hivyo
ndio maana nimeelekeza NEMC wapime washauri nini kifanyike,” alisema.
Aidha, Naibu Waziri Sima alisisitiza kuwa pamoja na
Serikali kualika wadau kuwekeza katika sekta ya viwanda lakini pia inao wajibu
wa kuhakikisha viwanda vinafanya shughuli zake bila kuathiri mazingira na
wananchi wanaozunguka.
Kwa upande wake Kaimu Meneja wa NEMC Kanda ya Mashariki
Ndimbumi Yoram alisema kumekuwepo na malalamiko kutoka kwa wananchi kuhusu
vumbi na moshi vinatoka kiwandani hapo.
Alitoa mwito kwa mwekezaji huyo ambaye pamoja na
kujikagua na kutoa ripoti kwa Baraza hilo lakini pia awaruhusu kufanya ukaguzi
wakati mashine zinafanya kazi ili waweze kushauri.
“Tunaona vumbi kwenye ambalo limetokana na kusaga mawe haya
ya kutengenezea chokaa lakini kwa sababu mitambo imezimwa hatuwezi kujua linatoka
wapi hivyo mwenye kiwanda awe muwazi aturuhusu tukague kikiwa kinafanya kazi
ili tujue vumbi linatoka wapi na tuweze kumshauri,” alisema Ndimbumi.
Nae Mkurugenzi wa kiwanda hicho Rashid Hamoud
aliishukuru Serikali kupitia kwa Naibu Waziri huyo kwa kutembelea na kuahidi
kutekeleza maelekezo yote yaliyotolewa.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na
Mazingira) Mhe. Mussa Sima (wa pili kulia) akiwa katika ziara ya kutembelea
kiwanda cha kutengeneza chokaa cha Neelkanth cha jijini Tanga kukagua
utekelezaji wa sheria ya mazingira.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na
Mazingira) Mhe. Mussa Sima (wa pili kulia) akiwa katika ziara ya kutembelea
kiwanda cha kutemgeneza chokaa cha Neelkanth cha jijini Tanga kukagua
utekelezaji wa sheria ya mazingira.
Ziara ya Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano
na Mazingira) Mhe. Mussa Sima (wa pili kulia) ikiendelea katika kiwanda cha
kutemgeneza chokaa cha Neelkanth cha jijini Tanga.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na
Mazingira) Mhe. Mussa Sima (wan ne kulia) akisikiliza taarifa kutoka kwa Mkuu
wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella mara baada ya kuwasili mkoani humo kuanza
ziara ya kikazi.
No comments:
Post a Comment