STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar
03.05.2020
RAIS wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, amemtumia salamu za rambirambi Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli kufuatia kifo cha Waziri wa
Katiba na Sheria Balozi Augustine Mahiga.
Balozi Mahiga alifariki
nyumbani wake Mjini Dodoma baada ya kuugua hafla ambapo alipofikishwa hospitali
tayari alikwishapoteza uhai na kuzikwa jana Mkoani Iringa.
Katika salamu hizo Dk.
Shein alisema amepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa ya kifo cha Waziri wa Katiba
na Sheria wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Agustine Mahiga
kilichotokea Mjini Dodoma.
“Kwa niaba ya watu wa
Zanzibar na Serikali natoa mkono wa pole na rambirambi kwako Mheshimiwa Rais,
familia ya marehemu pamoja na wananchi wote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
kwa msiba wa kuondokewa na kiongozi aliyekuwa na upendo wa nchi yetu”, ilieleza
sehemu ya salamu hizo za rambirambi alizozituba Dk. Shein.
Aidha, Dk. Shein alisema Balozi Mahiga ataendelea kukumbukwa kwa
mchango wake mkubwa katika kulinda na kutetea maslahi ya nchi katika shughuli
za kimataifa ikiwemo Afrika Mashariki, Umoja wa Afrika, Umoja wa Mataifa na
taasisi nyengine.
Dk. Shein alisema kuwa
Balozi Mahiga alikuwa mstari wa mbele katika kuleta maendeleo na kudumisha
umoja, amani na upendo katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kufuata
misingi ya Katiba na Sheria.
Rais Dk. Shein alimuomba
Mwenyezi Mungu awajaalie wafiwa na wananchi wote wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania moyo wa subira katika kipindi hichi cha msiba.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment