Habari za Punde

TIMU YA RAJAA FC YAWA TISHIO JIJINI DAR ES SALAAM


Timu ya soka ya Rajaa Fc ya Kariakoo jijini Dar es Salaam ikiwa kamili kukabiliana na timu yoyote ile


NA FREDY MGUNDA,IRINGA.
TIMU ya soka ya Rajaa Fc ya Kariakoo jijini Dar es Salaam inayoshiriki mashindao mbalimbali ya soka zinazondaliwa jijini Dar es Salaam na nje imejipanga kufanya vyema katika mashindano yoyote ikiwemo ligi ya kutafuta bingwa wa mkoa wa Dar es salaama katika kuelekea madaraja ya juu zaidi nchini.


Wakizungumza na waandishi wa habari,Kocha Mkuu wa timu hiyo, Kassim Ramadhani na viongozi wake Mohamed Abri walisema kuwa mara baada ya serikali kutangaza baadhi ya michezo kuendelea kama kawaida timu hiyo iko katika mazoezi makali yanayofanyika katika viwanja vya JK  na Uhuru taifa kujiwinda na mashindano yoyote yatakayojitokeza jijini Dar es Salaam. 

Kocha Ramadhani alisema kuwa wamejipanga katika suala zima la mazoezi kwani changamoto ilikuwa ni gonjwa la Covid 19 ila kwa sasa tumeanza mazoezi makali kwani wachezaji wengi walikuwa tu majumbani huku baadhi wakifanya mazoezi binafsi tofauti na timu hivvo kwa sasa ni mazoezi mwanzo mwisho. 

Alisema kuwa timu hiyo imekuwa timu mojawapo ndogo zenye uongozi uliojipanga vyema kuhakikisha inafanya vizuri kwenye ligi mbalimbali zinazoandaliwa jijini hapa kwa lengo la kujiweka vyema na kuanza maandalizi ya kutafuta bingwa wa mikoa inayotarajiwa kuanza wakati wowote. 

Alisema kuwa wachezaji wa timu hiyo wamekuwa katika hali nzuri na  ni vijana wenye nia ya kufanya vyema zaidi katika soka la Tanzania nje hivyo kuwa na njaa ya mafanikio chini ya uongozi bora kabisa wa Mkurugenzi wa timu  Mohamed Abri na nahodha wake Salim Salehe Abri. 

Aliongeza kuwa timu hiyo imekuwa ikishiriki mechi mbalimbali za ndani ya jiji na nje ya jiji ambapo walicheza mechi na timu ya Ligi Kuu ya Lipuli Fc mkoani Iringa na kuleta upinzani mkubwa hali ambayo iliwapa nguvu ya kuweza kufanya vyema katika mashindano yoyote watakayoshiriki. 

Kwa upande wake, Nahodha wa timu hiyo, Salim Salehe Abri alisema kuwa Klabu hiyo yenye wachezaji vijana na wenye hali wako tayari kwa mashindano yoyote watakayoshirki kwani wachezaji wako katika hali nzuri na kuwa na kila kitu ambacho wanahitaji kwa sasa ikiwemo vifaa na jezi za uhakika kushiriki mashindano mbalimbali. 

Abri aliwataka wachezaji wa timu hiyo kufanya mazoezi kwa moyo kwa lengo la kuiletea mafanikio timu biyo na kufanikisha malengo waliyojiwekea ya kuchukua ubingwa kwa kila mashindano watakayoshiriki jijini Dar es Salaam. 

Alisema kuwa kwa sasa timu hiyo kwa kushirikiana na uongozi na wachezaji wameweka mikakati ya kufanya vyema  nchini kwa ujumla hali ambayo inatokana na ushirikiano mzuri na  viongozi wa timu na wachezaji pamoja na mashabiki wanaowaunga mkono popote wanapokwenda 

Abri ambaye ameshiriki ligi mbalimbali za soka nchini amekuwa mstari wa mbele katika kuwapa moyo wachezaji chipukizi wa timu hiyo kuweza kuonyesha zaidi vipaji kwa lengo kujiuza zaidi katika ligi mbalimbali duniani kwa kupitia timu  ya Rajaa yenye mlengo wa kukuza vipaji za vya soka zaidi.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.