Habari za Punde

RAIS MHE. DKT. MAGUFULI ALIPOKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA WAZIRI MKUU MSTAAFU EDWARD LOWASSA NYUMBANI KWAKE CHAMWINO MKOANI DODOMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa wakati alipomkaribisha nyumbani kwake Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma jana mara baada ya hafla ya Chakula cha mchana aliyowaandalia Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa jana wakati alipomkaribisha nyumbani kwake Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma mara baada ya hafla ya Chakula cha mchana aliyowaandalia Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimsindikiza Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa mara baada ya mazungumzo yao nyumbani kwake Chamwino mkoani Dodoma baada ya hafla ya Chakula cha mchana aliyowaandalia Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli kushoto katika picha ya kumbukumbu na Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa aliyeambatana na Mkewe Mama Regina Lowassa nyumbani kwa Mhe.Rais Dkt. Magufuli

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa aliyeambatana na Mkewe Mama Regina Lowassa nyumbani kwa Mhe.Rais Dkt. Magufuli jana mara baada ya hafla ya Chakula cha mchana aliyowaandalia Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM. PICHA NA IKULU

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.