Na Mwandishi wetu-Dar
es Salaam.
Taarifa ya TIC
iliyosainiwa na Kaimu Afisa Habari na Uhusiano wa Taasisi hiyo Grace Semfuko
imesema kuna Taasisi inayojiita “Tanzania
Investments” ambayo inapatikana Jijini Mwanza imekuwa ikihamasisha watu
kuchangia kwa ajili ya kupata huduma za uwekezaji na kwamba tayari imeundwa
kundi la WhatsApp ambalo linahamasisha watu kujiunga na kupata huduma za
uwekezaji nchini.
“Ieleweke wazi kuwa
kundi hilo linafanya kazi zake kinyume cha sheria, na sisi tumeshatoa taarifa
kwenye vyombo vya kisheria ili waweze kushughulikiwa, wanatumia nembo na majina
ya kituo kuhalalisha utapeli wao, kituo cha uwekezaji tanzania ni Taasisi pekee
inayofanya kazi za kuhamasisha uwekezaji tukisaidiana na taasisi nyingine kama
EPZA na nyinginezo za Serikali zinazohusika na masuala haya” ilisema taarifa
hiyo.
“Kumezuka kundi la
WhatsApp linalojiita TANZANIA INVESTMENTS ambalo linajinasibu kusimamia
Uwekezaji nchini,kundi hili linajitambulisha kuwa linapatikana eneo la
Nyanguge, Magu, Mwanza, Kundi hili pia
linatumia majina na nembo ya Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), pamoja na
kuvunja sheria za nchikundi hili pia linafanya utapeli” ilisema taarifa hiyo.
Aidha,ilieleza kuwa
katika kusogeza huduma za uwekezaji maeneo yote nchini, TIC imeanzisha Ofisi za
Kanda saba (7) ili kuwafikia Wateja wake wote na kuwataka wadau kuzitumia ofisi
hizo.
Ilizitaja kanda hizo
kuwa ni pamoja na Kanda ya Kusini yenye Ofisi zake Mkoani Mtwara (Jengo la Mkuu
wa Mkoa) inayohudumia Mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma, Kanda ya Nyanda za Juu
Kusini yenye Ofisi zake Mkoani Mbeya
(Jengo la Benki ya NBC) inayohudumia Mikoa ya Iringa, Njombe, Mbeya, Songwe .
Kanda zingine ni
pamoja na ya Kaskazini yenye Ofisi zake Mkoani Kilimanjaro(Ofisi za Mkuu wa
Mkoa) inayohudumia Mikoa ya Kilimanjaro, Manyara, Arusha na Tanga, Kanda ya
Mashariki yenye Ofisi zake Dar es Salaam (Jengo la TIC Makao Makuu)
inayohudumia Mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Morogoro, Kanda ya Magharibi
yenye Ofisi zake Mkoani Kigoma (Jengo la Mkuu wa Mkoa) na inahudumia Mikoa ya
Rukwa, Katavi, Kigoma na Tabora.
Aidha zipo pia Kanda
ya Ziwa yenye Ofisi zake Mkoani Mwanza (Barabara ya Kenyatta), inayohudumia
Mikoa ya Mwanza, Mara, Kagera, Shinyanga,Geita na Simiyu na Kanda ya Kati yenye
Ofisi zake Dodoma (Jengo la Manispaa) inayohudumia Mikoa ya Morogoro, Dodoma na
Singida.
No comments:
Post a Comment