Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
(Sekta ya Mawasiliano), Dkt. Zainabu Chaula, akisisitiza jambo kwa wataalamu wa Shirika
la Mawasiliano Tanzania, Arusha (hawapo pichani) wakati wa ziara yake ya kukagua Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano
Na Prisca Ulomi, WUUM, Arusha
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Mawasiliano), Dkt. Zainabu Chaula,
jana amefanya ziara ya kukagua miundombinu ya Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano katika Mkoa wa
Arusha. Hii ni ziara yake ya kwanza
ya kukagua miundombinu hiyo tangu alipoteuliwa kuongoza Sekta hiyo ambapo ukaguzi huo utamuwezesha kusimamia vema Sekta hiyo.
Dkt.
Chaula akiwa ziarani mkoani humo,
amebaini nguvu ya miundombinu huo katika kuendesha shughuli za Serikali na kuhudumia wananchi ambapo taaasisi
za Serikali, sekta binafsi na wananchi wanatumia miundombinu na huduma za
mawasiliano katika masuala ya kiuchumi na kijamii
“Sekta ya Mawasiliano ni Sekta ya uchumi,
kimkakati, mtambuka na wezeshi na Serikali imetumia zaidi ya shilingi bilioni 630
kujenga miundombinu huo”, amesisitiza Dkt. Chaula.
Ameyasema hayo wakati alipokutana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, Richard Kwitega walipofika ofisini kwake kabla ya kuanza ziara ya kukagua muundombinu huo
Ameyasema hayo wakati alipokutana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, Richard Kwitega walipofika ofisini kwake kabla ya kuanza ziara ya kukagua muundombinu huo
Naye Kwitega alimueleza Dkt.
Chaula kuwa taasisi za Serikali zinatumia miundombinu huo pamoja na huduma za
mawasiliano kwa kiasi kikubwa ikiwemo uendeshaji wa mifumo mbalimbali ya Serikali ya ukusanyaji wa mapato,
utoaji wa huduma kwa wananchi na malipo mbalimbali kwa watumishi wa umma na wadau na amesema kuwa Sekta hii inategemewa na Serikali na wadau
wake
Kaimu Meneja wa TTCL Mkoa wa Arusha,
Emmanuel James amemweleza Dkt. Chaula kuwa katika Mkoa huo, TTCL
wana wateja wa aina mbalimbali ikiwemo taasisi za Serikali, sekta binafsi mfano benki,
kampuni za simu, hospitali, shule; huduma mtandao mathalani malipo mtandao kama vile
kulipia huduma za maji na umeme; ada; ukusanyajiwamapato, kodinatozombalimbali;
hudumaza afyamtandao, elimumtandaonabiasharamtandao
Wakiwa ziarani humo kwenye kituo cha
miundombinu huo, Namanga, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo ya Sekta ya Ujenzi, Arch.
Elius Mwakalinga ameulinganisha Mkongo huo na miundombinu ya barabara kwa kuwa Mkongo huo unabeba na kusafirisha mawasiliano ya
data na sauti na kupeleka kwa wateja ambapo Serikali imejenga vituo tisa mpakani mwa
Tanzania na nchi jirani ili kuweza kuzipatia nchi jirani huduma ya mawasiliano
Dkt.
Chaula amesema kuwa Serikali inategemea sana miundombinu ya Mkongo wa Taifa Mawasiliano katika kuendesha shughuli zake na kuhudumia wananchi hivyo ametoa
rai kwa TTCL kuendesha miundombinu huo kwa maslahi ya taifa
Imetolewa na Kitengo
cha Mawasiliano Serikalini,
Wizara ya Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Ujenzi),
Arch. Elius Mwakalinga akinyoosha mkono kwenye betri za
Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano kwenye kituo cha Nananga, Arusha
wakati wa ziara ya kukagua miundombinu huo. Wa pili kushoto ni Dkt. Zainabu Chaula,
Katibu Mkuu wa Wizara hiyo wa Sekta ya Mawasiliano
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano
(Sekta ya Mawasiliano), Dkt. Zainabu Chaula (wa pili kulia) na wa Sekta ya Ujenzi
(wa tatu kulia), Arch. Elius Mwakalinga wakimsikiliza Kaimu Meneja wa Shirika la
Mawasiliano Tanzania wa Arusha, Emmanuel James
wakati wakikagua miundombinu ya Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano kituo cha
Namanga mkoani humo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
(Sekta ya Mawasiliano), Dkt. Zainabu Chaula na wa Sekta ya Ujenzi, Arch.
Elius Mwakalinga wakimsikiliza Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, Richard Kwitega walipofika ofisini kwake kabla ya kuanza ziara ya kukagua miundombinu ya Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano mkoani humo.
No comments:
Post a Comment