Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt.
Hassan Abbasi akisisitiza jambo wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari Agosti
7, 2020 Jijini Dodoma kuhusu Serikali ya Awamu ya Tano kuvunja rekodi ya ukuaji wa uchumi wa nchi katika kipindi
cha miaka minne ya utawala wake sambamba na kupunguza mfumuko wa bei kutoka wastani wa asilimia 9.2 mwaka
2015 hadi asilimia 4.3 mwaka 2019/2020.
Na.
Immaculate Makilika na Frank Mvungi- MAELEZO
Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli imeendelea kuvunja
rekodi ya ukuaji wa uchumi wa nchi katika kipindi cha miaka minne ya utawala
wake sambamba na kupunguza mfumuko wa bei kutoka wastani wa
asilimia 9.2 mwaka 2015 hadi asilimia 4.3 mwaka 2019/2020.
Akizungumza
katika Mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dodoma, Katibu Mkuu Wizara ya
Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni semaji Mkuu wa Serikali, Dkt.
Hassan Abbasi alisema sasa pato la Taifa (GDP) ni kubwa kuliko miaka yote
tangu uhuru na kufanya uchumi wa Tanzania kuwa wa 10 barani Afrika na mfumuko
wa bei kuwa mdogo kuliko wakati wowote katika historia ya Tanzania.
“Katika
kipindi cha miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Tano, pato la Taifa limekua kwa
wastani wa shilingi trilioni 124 kwa mwaka ikilinganishwa na wastani wa
shilingi trilioni 52.9 kwa mwaka katika kipindi cha Awamu ya Nne” alieleza Dkt.
Abbasi.
Aliongeza
kuwa Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Magufuli imesimamia na kuhakikisha
Tanzania inaendelea kuwa ukuaji mzuri wa uchumi. Aidha, katika miaka minne
(2016-2019) uchumi wa Tanzania umekuwa kwa wastani wa asilimia 6.9 kwa mwaka,
wastani ambao ni mkubwa ikilinganishwa na Awamu zote.
Dkt.
Abbasi alisema kuwa msingi mwingine muhimu katika ukuaji wa uchumi wa nchi na
katika kutekeleza azma ya kujitegemea umekuwa ni kuongeza mapato ya Serikali
kutoka wastani wa shilingi bilioni 850 mwaka 2015 hadi shilingi trilioni 1.3
mwaka 2016, 2018/19 na Julai, 2019 hadi Juni, 2020 umefikia wastani mpya wa
shilingi trilioni 1.5 (ambapo kwa mwezi Disemba, 2019 na Juni 2020 imekusanywa trilioni 1.9 mtawalia).
Serikali
ya Awamu ya Tano, imefanikiwakuongeza mapato yasiyo ya kodi yameongezeka kutoka
shilingi bilioni 688.7 mwaka 2014/2015 hadi kufikia shilingi trilioni 2.4 mwaka
2018/2019. Ambao kuongezeka kwa mapato hayo mapato yasiyo ya kodi ni matokeo ya
kubana mianya ya kukwepa kodi, muamko wa wananchi kulipa kodi, usimamizi mzuri
wa Wizara ya Fedha, TRA na Serikali kwa ujumla.
Katika
hatua nyingine, Dkt. Abbasi alisem kuwa Taasisi za kimataifa zimeendelea
kusifia ukuji wa uchumi wa nchi ambapo Septemba 30, 2019 Benki ya Dunia iliitaja
Tanzania kuwa ni nchi yenye uchumi unaokuwa kwa wastani wa asilimia 6 hadi 7 kwa mwaka katika kipindi
cha miaka 10.
“Benki
ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) imeitaja Tanzania kuwa nchi yenye uchumi jumuishi
wenye kuzingatia maslahi ya umma, uwekezaji imara na unaokuwa pamoja na
kuongezeka kwa mauzo ya bidhaa za nje. Aidha, Machi, 2020 Shirika la Fedha Duniani
limesema hali ya uchumi wa Tanzania umeendelea kuwa imara ukikua kwa zaidi ya asilimia
6, mfumuko wa bei ukiwa chini ya asilimia 5 na akiba ya fedha za kigeni ikiwa
ya kutosheleza na deni la taifa likiwa himilivu.” Alisema Dkt. Abbasi
Halikadhalika
jarida la Forbes linaitaja Tanzania kuwa nchi ambayo uchumi wake umekua kwa
wastani wa aslimia 6 hadi asilimia 7 kwa mwaka kutokana na matumizi mazuri ya rasilimali zake na
utalii kati ya mwaka 2009 hadi 2017.
Fauku
ya hayo, Dkt. Abbasi alisema kuwa miaka mitano ijayo Serikali itaendelea kuweka
sera, mipango na mikakati, kusimamia na kulinda misingi ya uchumi na nchi
kuendelea kuwa katika uchumi wa kati.
Aidha,
Msemaji Mkuu wa Serikali amewataka watanzania kushiriki katika maendeleo ya
uchumi kwa kufanyakazi kwa bidii, kuepuka
rushwa na uvivu kazini, kulipa kodi na kushiriki
kutumia fursa zinazojitokeza katika
ukuaji wa uchumi na kutoa maoni kwa Serikali katika kuboresha uchumi wa nchi.
No comments:
Post a Comment