Mkurugenzi Mkuu LATRA
Gilliard Ngewe akimkabidhi Henry Machoke, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara
TRC andiko la nauli zilizoidhinishwa.
Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imetangaza nauli za treni ya abiria itakayofanya safari zake kutoka Moshi mjini hadi Arusha na kurudi Moshi. Akizungumza na waandishi wa habari Mkoani Arusha leo tarehe 29 Septemba, 2020, Mkurugenzi Mkuu wa LATRA Gilliard Ngewe amesema nauli hizo zimetangazwa kufuatia Shirika la Reli Nchini (TRC) kuwasilisha maombi ya nauli hizo, ambapo LATRA ilifanya mikutano ya kupokea maoni ya wadau, kisha kufanya uchambuzi wa maoni hayo pamoja na kuchambua mchanganuo uliowasilishwa na TRC.
Kwa
mujibu wa kifungu cha 21 (2) (b) cha Sheria ya LATRA namba 3 ya 2019, baada ya
mchakato wa uchambuzi kukamilika, Bodi ya Wakurugenzi ya LATRA imeidhinisha
nauli hizo na kuainisha nauli zitakazotumika kwa usafiri wa treni ndani ya mikoa
hiyo na nje ya mikoa kama inavyoonekana katika jedwali.
Nauli zilizoidhinishwa na LATRA zikionesha
mchanganuo wa vituo vya ndani nan je ya mikoa husika
|
KUTOKA MOSHI
KWENDA |
Umbali (KM) |
NAULI
KWA MADARAJA HUSIKA (SHS): |
|
Daraja la
tatu |
Pili kukaa |
|||
1 |
RUNDUGAI |
22 |
1,000 |
1,500 |
2 |
KIKULETWA |
31 |
1,000 |
1,500 |
3 |
KIA |
37 |
1,000 |
1,500 |
4 |
USA
RIVER |
62 |
1,500 |
2,000 |
5 |
TENGERU |
65 |
1,500 |
2,000 |
6 |
CHEKERENI |
75 |
1,500 |
2,000 |
7 |
NJIRO |
82 |
1,500 |
2,000 |
8 |
ARUSHA |
86 |
1,500 |
2,000 |
|
KUTOKA
ARUSHA KWENDA |
Umbali (KM) |
NAULI KWA
MADARAJA HUSIKA (SHS): |
|
Daraja la
tatu |
Pili kukaa |
|||
1 |
NJIRO |
4 |
1,000 |
1,500 |
2 |
CHEKERENI |
11 |
1,000 |
1,500 |
3 |
TENGERU |
21 |
1,000 |
1,500 |
4 |
USA
RIVER |
24 |
1,000 |
1,500 |
5 |
KIA |
49 |
1,500 |
2,000 |
6 |
KIKULETWA |
55 |
1,500 |
2,000 |
7 |
RUNDUGAI |
64 |
1,500 |
2,000 |
8 |
MOSHI |
86 |
1,500 |
2,000 |
Nauli
za wanafunzi kutoka mwanzo hadi mwisho wa safari ni Sh. 300.00 kwa daraja la
tatu, na Sh 400.00 kwa daraja la pili kukaa.
Wakati huo huo, LATRA imeiagiza TRC kutekeleza masuala mbali mbali ikiwa ni pamoja na kutoa elimu ya usalama kwa wadau husika, kutumia mfumo wa tiketi za kielektroniki, kutoa ratiba za safari kwa umma, kutekeleza hatua za usalama kudhibiti msongamano wa abiria, kuboresha miundombinu na huduma za kijamii, kuweka kitengo cha huduma kwa wateja na kutangaza nauli zilizoidhinishwa katika vyombo mbalimbali vya habari ili ziwafikie wadau wengi zaidi.
No comments:
Post a Comment