Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein Shein Amejumuika na Waumini wa Kiislam Zanzibar Katika Maulidi ya Kuzaliwa Mtume Muhammad (S.A.W) Yaliofanyika Katika Viwanja Vya Maisara Suleiman Jijini Zanzibar 18/10/2020.ma AT

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk. Ali Mohamed Shein akiwa na Viongozi wa Serikalina Dini wakiwa wamesimama  wakati Madrassatul Qullatenia Mwanakwerekwe wakitowa Salamu ya Rais baada ya kuwasili katika viwanja vya mpira ya Maisara Suleiman kuhudhuria hafla ya Maulidi ya Kuadhimisha Kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W) yaliofanyika jana usiki 18/10/2020.
MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein na (kushoto kwa Mama ) Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan, wakijumuika na Waumini wa Dinui ya Kiislam katika hafla ya Maulidi ya Kuzaliwa kwa Mtume Muhammad yaliofanyika katika viwanja vya Maisara Suleiman Jijini Zanzibar, wakiwa wamesimama wakati Madrassatul Qullatenia ya Mwanakwerekwe Jijini Zanzibar wakitowa Salamu ya Rais.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Alhajj Dk. Ali Mohamed  Shein, akiwa katika viwanja vya Maisara Suleiman akihudhuria hafla ya Maadhimisho ya Kuzaliwa Mtume Muhammad (S.A.W) yaliofanyika jana usiku 18/10/2020 na (kulia kwa Rais) Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Mahmoud Mussa Wadi.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Alhajj Dk. Ali Mohamed  Shein, akitia ubani  kumainisha kuyafungua Maulidi ya Kuadhimisha Kuzaliwa kwa MtUME Muhammad (S.A.W) yaliofanyika katika viwanja ya Maisara Suleiman Jijini Zanzibar, yalifanytika jana usiku

Ustadh Khamis Ali Tano kutoka Donge Mchangani Mkoa wa Kaskazini Unguja akisoma Barzanji Mlango wa Kwanza, wakati wa hafla ya Maulidi ya Kuadhimisha kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W) yaliofanyika jana usiku 18/10/2020 katika viwanja vya Maisara Suleiman Jijini Zanzibar



SHEIKH Abdullah Hamid kutoka Chuo cha Kiislam Mazizini Zanzibar akisoma Tafsi ya Quran tukufu (Suratul Aaraf Aya ya 156b -158) wakati wa hafla ya Maadhimishi ya Maulidi ya Kuzaliwa Mtume Muhammad (S.A. W) yaliofanyika katika viwanja vya Maisara Suleiman Jijini Zanzibar.



BAADHI ya Waumini wa Dini ya Kiislam Zanzibar wakishiriki katika hafla ya Maulidi ya Kuzaliwa Mtume Muhammad (S.A.W) yaliofanyika katika viwanja vya Maisara Suleiman Jijini Zanzibar.













 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.