Habari za Punde

Mgombea Urais wa Zanzibar Kwa Tiketi ya CCM Mhe.Dk. Hussein Mwinyi Akiwasili Katika Uwanja wa Jamuhuri Makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja leo 1/10/2020.

Mgombea Urais wa Zanzibar kwa Tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe. Dk. Hussein Mwinyi akiwasili katika Uwanja wa Jamuhuri kuhudhuria mkutano wake wa Kampeni ya kugombea Urais wa Zanzibar uliofanyika leo katika uwanja huo Mkoa wa Kusini Unguja. akiwa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Abdalla Juma Mabodi wakielekea katika jukwaa kuu.

Wanachama wa CCM Mkoa wa Kusini Unguja wakimshangilia mgombea Urais wa Zanzibar Mhe.Dk. Hussein Ali Hassan Mwinyi wakati akiwasili katika uwanja wa jamuhuri makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja kuhudhuria mkutano wa kampeni uliofanyika leo 1/10/2020.

Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe.Dk. Hussein Mwinyi akisalimiana na Katibu Mkuu wa CCM Dkt, bashiru Ally alipowasili katika jukwaa kuu la viongozi katika uwanja wa Jamuhuri Makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja wakati wa mkutano wake wa kampeni katika Mkoa huo leo. 
Rais Mstaaf wa Tanzania Mhe.Ali Hassan Mwinyi akisalimiana na Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe.Dk. Hussein Ali Hassan Mwinyi alipowasili katika jukwaa kuu la viongozi wakati wa hafla ya mkutano wa kampeni ya mgombea Urais wa Zanzibar uliofanyika katika uwanja wa mpira wa jamuhuri Makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja.
Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Mhe.Dk. Husseinn Mwinyi akisalimiana na Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe.Zuberi Ali Maulid alipowasili katika jukwaa kuu la viongozi katika uwanja wa mpira wa Jamuhuri Makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja leo 1/10/2020.
Wanachama wa CCM wakishingilia wakati wa mkutano wa Kampeni yac Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Mhe.Dk. Hussein Mwinyi wakati akiwasili katika uwanja jamuhuri makunduchi. 



 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.