Habari za Punde

Mkutano wa Kampeni Mgombea Urais wa Tanzania Kwa Tiketi ya CCM Mhe.Dkt. John Magufuli Viwanja Vya Mnazi Mmoja Jijini Zanzibar leo 3/10/2020

 

Mgombea Urais wa Zanzibar kwa Tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Mhe,.Dk. Hussein Ali Hassan Mwinyi akiwasalimia Wananchi na WanaCCM alipowasili katika viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Zanzibar kuhudhuria Mkutano wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli uliofanyika leo Zanzibar 3/10/2020, na kuhudhuriwa na Umati wa Wanachama wa CCM Zanzibar.

Mgombea Urais wa Tanzania kwa Tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili katika Uwanja wa Mzani Mmoja Jijini Zanzibar kuhudhuria Mkutano wa Kampeni wa CCM uliofanyika leo 3/10/2020, akiwapungia mkono Wanachama wa CCM waliohudhuria mkutano huo.

Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi Zanzibar wakishangilia wakati wa kuingia Wagombea Urais wa Zanzibar Mhe.Dk. Hussein Mwinyi na Mgombea Urais wa Tanzania Mhe.Dkt. John Magufuli katika viwanja vya Mnazi Mmoja kuhudhuria mkutano wa kampeni wa Mgombea Urais wa Tanzania Mhe. Magufuli uliofanyika kayika uwanja wa Mnazi Mmoja Jijini Zanzibar leo.

Rais Mstaaf wa Tanzania Awamu ya Pili Mhe.Ali Hassan Mwinyi akisalimiana na Mgombea Urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ambae pia ni Mwenyekiti wa CCM Taifa Mhe.Dk. John Pombe Magufuli  alipowasili katika jukwaa kuu la viongozi katika uwanja wa Mnazi Mmoja kuhudhuria mkutano wa kampeni ya Mgombea Urais wa Tanzania Mhe Dkt.Magufuli leo.

Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein na Mgombea Urais wa Tanzania Mhe Dk. John Magufuli na Viongozi wengine wakiitikia dua kabla ya kuaza kwa mkutano wa kampeni katika Uwanja wa Mnazi Mmoja leo 2/10/2020.

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Zanzibar ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein akiwahutubia Wananchi wa Zanzibar katika mkutano wa kampeni ya Mgombea Urais wa Tanzania uliofanyika katika Uwanja wa Mnazi Mmoja Jijini Zanzibar leo. kabla ya kumkaribisha Mgombea Urais wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli kuwahutubia Wananchi wa Zanzibar. na kuwaomba kura. 

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Zanzibar ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein akiwahutubia Wananchi wa Zanzibar katika mkutano wa kampeni ya Mgombea Urais wa Tanzania uliofanyika katika Uwanja wa Mnazi Mmoja Jijini Zanzibar leo. kabla ya kumkaribisha Mgombea Urais wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli kuwahutubia Wananchi wa Zanzibar. na kuwaomba kura. 

Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Mwinyi akiwahutubia Wananchi wa Zanzibar katika Uwanja wa Mnazi Mmoja Jijini Zanzibar leo 3/10/2020, na kuwaomba Kura na kumuombea Kura Mgombea Urais wa Tanzania Mhe.Dkt. John Magufuli na Wabunge,Wawakilishi na Madiwani wote wa CCM Zanzibar.

Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Mhe.Dk. Hussein Mwinyi akisisitiza jambo wakati akihutubia katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika Uwanja wa Mnazi Mmoja Jijini Zanzibar, akitangaza Sera za Chama Chake katika mkutano huo uliofanyika leo 3/10/2020.

Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi  Zanzibar wakishangilia wakati wa mkutano wa kampeni wa Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Mhe.Dk. Hussein Mwinyi.(hayupo pichani) uliofanyika katika Uwanja wa Mnazi Mmoja Jijini Zanzibar  leo 3/10/2020.

Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya CCM ambae pia ni Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Magufuli na Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Zanzibar ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, wakipiga makofi wakati Mgombea wa Urais wa Zanzibar Mhe.Dk. Hussein Mwinyi akiwahutubia Wananchi katika Uwanja wa Mnazi Mmoja Jijini Zanzibar leo wakati wa mkutano wa kampeni ya Mgombea Urais wa Tanzania.

Mgombea Urais wa Tanzania ambae pia ni Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.John Pombe Magufuli akisisitiza jambo wakati akihutubia katika mkutano wake wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa Mnazi Mmoja Jijini Zanzibar leo.
Wake wa Viongozi wakifuatilia mkutano wa kampeni ya Mgombea Urais wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli uliofanyika katika Uwanja wa Mnazi Mmoja Jijini Zanzibar leo.
Mwanachama wa CCM Zanzibar ak,imshangilia Mgombea Urais wa Tanzania Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli akiwahutubia katika mkutano wake wa Kampeni uliofanyika katika Uwanja wa Mnazi Mmoja Jijini Zanzibar leo. 
Umati wa Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi Zanzibar wakifuatilia mkutano wa kampeni wa Mgombea Urais wa Tanzania Mhe.John Magufuli uliofanyika katika Uwanja waMnazi Mmoja Jijini Zanzibar leo 3/10/2020. 
Mwanachama wa CCM akiwa na bango la picha ya Mgombea Urais wa Zanzibar Mhe.Dk. Hussein Mwinyi na picha yao wa Kikundi cha Team Mwinyi Kwanza wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika Uwanja wa Mnazi Mmoja leo.
Mgombea Urais wa Zanzibar Mhe.Dkt. John Magufuli akiserebuka na Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya Bongo Flava Zuchu wakati wa mkutano wake wac kampeni uliofanyika katika Uwanja wa Mnazi Moja Jijini Zanzibar.
Mgombea Urais wa Tanzania Mhe.John Magufuli Mgombea Urais wa Zanzibar.Mhe.Dk Hussein Mwinyi na Makamu Mweyekiti wa CCM Zanzibar ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein wakisakata rumba wakati msanii Zuchu akitowa burudani katika mkutano wa kampeni ya Mgombea Urais CCM iliofanyika katika Uwanja wa Mnazi Mmoja Jijini Zanzibar.
Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi Zanzibar wakishangilia katika mkutano wa kampeni ya CCM uliofanyika katika Uwanja wa Mnazi Mmoja Jijini Zanzibar.

Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein akisalimiana na Wanachama wa CCM baada ya kumalizika kwa mkutano wa kampeni ya mgombea Urais wa Tanzania uliofanyika katika Uwanja wa Mnazi Mmoja Jijini Zanzibar.

Mgombea Urais wa Zanzibar Mhe.Dk. Hussein Mwinyi akisalimiana na Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi baada ya kumalizika kwa mkutano wa kampeni ya Mgombea Urais wa Tanzania Mhe.Dkt. Hussein Mwinyi uliofanyika katika Uwanja wa Mnazi Mmoja Jijini Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.