RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapainduzi Dk. Ali Mohamed Shen
amewataka wafanyakazi wa Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Pemba, kufanya kazi kwa bidii na kuongeza kasi na ari ya utendaji kwani Ofisi
hiyo ina heshima ya pekee.
Rais Dk. Shein aliyasema hayo leo katika uzinduzi wa jengo la Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi iliyopo Chake Chake, Mkoa wa Kusini Pemba iliyokwenda sambamba na uzinduzi wa nyumba za Ikulu huko Micheweni, Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Rais Dk. Shein aliwataka wafanyakazi wa
Ofisi hiyo kuendelea kulinda hadhi na heshima ya Ofisi hiyo na kuwataka kuendelea
kushirikiana huku akisisitiza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea
kuwawekea mazingira mazuri ya kazi wafanyakazi wake wote.
Rais Dk. Shein alitoa pongezi kwa uongozi
wa Ofisi ya Rais na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, ukiongozwa na Waziri
Issa Haji Gavu kwa kusimamia vizuri kazi za ujenzi wa jengo hilo hadi
kukamilika na leo kuzinduliwa.
Pia, aliwapongeza wakandarasi wazalendo
na kutumia fursa hiyo kumpongeza Msanifu wa Majengo ambaye pia, ni Meneja wa
Majengo Ikulu Mohamed Abdulrahman Machungwa pamoja na Ramadhan Mussa Bakari
ambaye ni Mkurugenzi wa Wakala wa Majengo Zanzibar (ZBA) ambayo ndio iliyojenga
jengo hilo.
Alisema kuwa nyumba za eneo hilo la Ikulu
zilikuwa zimechakaa sana na ndipo ndani ya mika kumi iliyopita Ofisi hiyo
ilianza kazi ya kuzifanyia ukarabati na nyengine kuzijenga upya.
Alisema kuwa kwa upande wa Pemba Ofisi
hiyo imefanya kazi kubwa ikiwa ni pamoja na kuimarisha Ikulu ya Mkoani, kujenga
Ikulu ya Micheweni pamoja na nyumba za Ikulu za eneo hilo na jengo hilo jipya
la Ofisi lililozinduliwa hivi leo.
Rais Dk. Shein alisisitiza kwamba majengo
yote hayo yamejengwa kwa fedha za Serikali pamoja na yale yote aliyoyazindua
hivi karibuni zikiwemo nyumba za Kwahani, Maduka ya biashara Michenzani, nyumba
za Mbweni pamoja na ofisi kadhaa za Serikali zikiwemo zile za Gombani Pemba.
Alisisitiza haja ya kutunzwa kwa jengo
hilo ili liweze kutumika kwa muda mrefu na kuwataka wafanyakazi waharakishe
kuhamia ili kuanza kazi huku akisisitiza kuwa thamani mpya zitaingizwa hapo baadae
na hivi sasa watumie walizonazo.
Alieleza kuwa lengo la kujenga ofisi mpya
na nzuri ni kwa ajili ya kuwapatia wafanyakazi maeneo mazuri ya kufanya kazi na
kuwaweka katika mazingira bora ya kazi ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi
zaidi.
Alisema kuwa hatua hiyo itawapelekea
wafanyakazi kuridhika kwani iwapo wafanyakazi wataridhika ndipo wataweza
kufanya kazi vyema.
Rais Dk. Shein alisisitiza haja ya
kuyatunza na kuyalinda mazingira na kueleza kwamba kila mmoja ana jukumu la
kulitunza na kulienzi jengo hilo na kutaka majengo yote ya Ikulu yaendelezwe na
yatunzwe.
Alieleza azma ya Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar ya kuanzisha Wakala wa Nyumba na Majenzi, Shirika la Nyumba pamoja na
kuanzisha Kampuni ya Majenzi ya Serikali ambayo itasaidia kwa kiasi kikubwa
katika kupunguza gharama za ujenzi kwa majengo ya Serikali.
Alisema kuwa uzoefu wa Serikali kujenga
majengo yake wenyewe unatokana na uzoefu wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Hayati
Mzee Abeid Amani karume ambapo katika uongozi wake majengo mengi yalijengwa kwa
gharama za Serikali.
Alitumia fursa hiyo kuwaongeza wafanya
kazi wote wa Ofisi ya Rais wa Unguja na Pemba pamoja na wale wote waliowahi
kufanya kazi katika Ofisi hiyo na hivi sasa wamehamishiwa Ofisi nyengine.
Nae Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Issa Haji Ussi Gavu alitoa shukurani kwa Rais
Dk. Shein kwa maelekezo yake mbali mbali pamoja na miongozo yake katika kuhakikisha
ujenzi unafanyika vyema katika majengo yote ya Ikulu za Pemba, Unguja, Dar es
Salaam na Dodoma.
Waziri huyo alitoa shukurani kwa
mashirikiano makubwa yaliyofanyika katika ujenzi huo na kumpongeza Katibu wa
Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi kwa mashrikiano yake pamoja na
Maafisa Wadhamini wote walioshiriki.
Alitoa shukurani kwa Rais Dk. Shein kwa
kuelekeza na kuhakikisha kuwa jengo hilo linakamilishwa katika uongozi wa Rais
Dk. Shein.
Mapema katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Salum Maulid Salum alitoa shukurani kwa Rais
Dk. Shein kwa kutia shime ya kujienga jengo hilo na kulimaliza kwa wakati.
Aidha, maamuzi ya ujenzi wa jengo hilo
yanaenda sambamba na utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), ya
mwaka 2015-2020.
Aliongeza kuwa matayarisho ya ujenzi wa
jengo hilo yalianza mwezi Novemba 2018 ambapo Wakala wa Majengo Zanzibar (ZBA)
walilikagua eneo hilo kimazingira ili kuhakikisha hawaharibu mandhari ya eneo
hilo ambalo asili yake lipo katibu na ufukwe wa bahari.
Vile vile, Katibu Mkuu huyo alisema kuwa
Wakala wa Majengo walichukua sampuli ya udongo wa eneo hilo kwa ajili ya vipimo.
Alisema kuwa michoro ya awali ya jengo
hilo ilitayarishwa na Msanifu wa Majengo Ikulu Mohamed Abdulrahman maarufu
Machungwa ambae pia ni Meneja wa Majengo
Ikulu ambapo michoro hiyo baadae iliimarishwa na Wakala wa Majengo baada ya
makubaliano na Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.
Katibu Mkuu huyo alieleza kuwa jengo hilo
lina eneo la mita za mraba 654(sqm) ambapo kutokananna hali ya udongo wa eneo
hilo msingi wa jengo una urefu wa mita 2na
umeongezwa nguvu ya zege na nondo zilizolazwa kwa mfano wa kiatu cha
kusimamia jengo.
Alisema kuwa sehemu ya chini ya jego hilo
lina vyumba vya Ofisi saba, ukumbi wa mkutano na ukumbi wa kusalia wageni
ambapo pia kuna huduma za kutosha zikiwemo mazingatio ya watu wenye ulemavu.
Kwa mujibu wa maelezo ya Katibu Mkuu,
sehemu ya juu ina vyumba sita vya Ofisi, ukumbi mkubwa wa mikutano na ukumbi wa
kusubiria wageni ambapompia jengo hilo limezingatia masuala ya usalama wa moto
kwa watumiaji wake na limezingatia masuala ya usalama wa moto kwa watumiaji
wake na limewekewa njia ambazo ni rahidi kutumika wakati wa uokozi.
Alisema kuwa jengo hilo litakuwa na ‘lift’
ambayo hivi sasa ipo katika matengenezo na inategemewa kuwekwa baada ya wiki 15
ambapo jengo hilo linaweza kuongezwa ghorofa mojaa ya ziada kwa matumizi ya
baadae.
Sambamba na hayo, alisema kuwa gharama za
jengo hilo zimetolewa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ndio iliyotoa fedha
za ujeni huo ambapo iliingia mkataba na Wakala wa ujenzi kulijenga kwa TZS 528,465,875.
Gharama nyengine za nyongeza ni ya kuweka
lift na vifaa vyengine kama vile vipoza hewa pamoja na vifaa vya umeme na vya
kuzimia moto vitagharimu TZS 77,400,000.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail:
rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment