Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na viongozi mbalimbali mara baada ya kuwaapisha Mawaziri pamoja na Manaibu Waziri katika hafla iliyofanyika Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma
Na
Immaculate Makilika-MAELEZO
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amewataka mawaziri kutoogopa
kufanya maamuzi kwa kuogopa kufanya
uamuzi mabaya.
Akizungumza leo, Ikulu
Chamwino Dodoma mara baada ya kuwaapisha
mawaziri 21 na manaibu waziri 22, Rais Magufuli alisema sasa mawaziri
wanatakiwa kufanya maamuzi bila kuogopa
kukosea. “Ni vizuri ukafanye uamuzi mbaya kuliko kutokufanya uamuzi, unashindwa
kutoa uamuzi kwasababu hutaki uonekane mbaya, katika kipindi cha miaka mitano
iliyopita miradi ya maji zaidi ya 1,400 imekamilika, kwa hiyo mkafanye kazi, kafanyeni
uamuzi hasa unaohusu maslahi ya taifa”, alisema Rais Magufuli
Aidha, Rais Magufuli
amewataka mawaziri na viongozi wa Serikali kuzingatia
uadilifu na kuhakikisha kuwa maagizo na maelekezo ya Serikali yanafuata
utaratibu. “Ndani ya Serikali sasa hivi kuna ugonjwa mmoja wa ajabu, kwamba
hata mawasiliano yanatumwa kwenye ‘group
za WhatsApp, barua nyingine ni za siri na zinaishia kuvuja. Tuzingatie
maadili ya viapo vyetu na tufanye kazi zetu kwa uadilifu mkubwa, Serikali
hufanya kazi kwa maandishi”, alisisitiza Rais Magufuli.
Kuhusu somo la
historia, Rais Magufuli ameitaka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
kuhakikisha kuwa somo hilo linakuwa somo la lazima kufundishwa mashuleni ili
wanafunzi waweze kujua historia ya nchi yao.
“Nataka wanafunzi wetu
wafundishwe historia ya Tanzania na hii itasaidia kujenga uzalendo, vijana
hawajui historia ya nchi yetu, inawezekana masomo haya yatasaidia kujua jinsi
wageni walivyokuja wakadanganya wazee wetu”, alisisitiza Rais Magufuli.
Katika hatua nyingine,
Rais Magufuli alizungumzia changamoto zilizopo katika sekta mbalimbali ikiwemo
matumizi mabya ya fedha za umma ambapo alimtaka Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kufanya uchunguzi wa matumizi mabaya ya
fedha yaliyofanywa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa kununua
gari la gharama ya zaidi ya shilingi milioni 400.
Halikadhalika, Rais
Magufuli alisema kuwa katika kipindi cha
miaka mitano iliyopita vijiji 9,880 vilipata umeme na katika kipindi cha miaka
mitano ijayo vijiji 2,338, vilivyobaki pia vipate umeme, sambamba na kuanza
mradi wa uzalishaji megawati 350 za umeme
wa maji mkoani Njombe zitakazoingizwa kwenye Gridi ya Taifa.
Vilevile, Rais Magufuli
alimtaka Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Innocent Bashungwa
kuhakikisha kero za wasanii na wanamichezo
zinapatiwa ufumbuzi ikiwemo kusaidia wasanii kupata haki zao.
Katika hatua nyingine,
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan
aliwataka mawaziri kafanya kazi kwa
bidii, ili kutimiza matumaini ya wananchi katika kutatua kero mbalimbali zinazowakabili.
Naye, Waziri Mkuu,
Kassim Majaliwa alisema kuwa mawaziri, wameapa kumsaidia mhe. Rais kazi na jukumu
kubwa ni kufanya kazi kwa kuwatumikia
watanzania. “Tunahitaji kuona matokeo ya kazi maana miongozo tayari tunayo.
Twende tukachape kazi”, alisema Waziri Mkuu Majaliwa.
No comments:
Post a Comment