Habari za Punde

Makamu wa Rais akutana na kamati za Maendeleo Kizimkazi

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Wajumbe wa Kamati  za Maendeleo za Kizimkazi Mkunguni, Kizimkazi Dimbani na Kibuteni pamoja na  Watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kusini Unguja, lengo la kikao hicho ni kutathmini Miradi mbalimbali ya maendeleo kwa kipindi kilichopita na kipindi kijacho. kikao hicho kimefanyika leo  Januari 07, 2021 katika Ukumbi wa mikutano wa Shule ya Sekondari Kizimkazi Mkoa wa Kusini Unguja. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Baadhi ya wajumbe wa Kamati za Maendeleo za Kizimkazi Mkunguni, Kizimkazi Dimbani na Kibuteni  wakimsikiliza kwa makini Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ( hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao  leo  Januari 07, 2021 katika Ukumbi wa mikutano wa Shule ya Sekondari Kizimkazi Mkoa wa Kusini Unguja. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.