RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akishuhudia utiaji wa Saini ya Maelewano
(MOU) Mradi wa Ufuaji wa Umeme kwa Nishati ya Gesi, (kulia kwa Rais) Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Tangen Bw.
Allan Kesseler na kwa upande wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar umesainiwa na
Katibu Mkuu Wizara Maji Nishati na Madini Zanzibar Dkt. Mngereza Mzee Miraji
(kushoto kwa Rais) hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzin Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akishuhudia utiaji wa Saini ya Maelewano (MOU) na Kampuni ya Tangen &Intertorco Group ya Mradi wa Ujenzi wa Bandari ya Uvuvi Unguja na Mkoani Pemba, kwa upande wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar umesainiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Dkt. Aboud Suleiman Jumbe (kushoto kwa Rais) na(kulia kwa Rais) Mwakilishi wa Kampuni ya Tangen &Intertorco Group Bw. Michael Angaga, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar
MWAKILISHI wa Kampuni ya Tangen & Intertorco
Bw. Michael Angaga akitowa maekezo ya Mradi wa Ujenzi wa Bandari ya Uvuvi Mpiga
Duri Unguja na Mkoani Pemba, wakati wa hafla hiyo iliofanyika katika ukumbi wa
Ikulu Jijini Zanzibar.
MKURUGENZI Mtendaji wa Kampuni Tangen & Intertorco
Bw. Allan Kessler akizungumza na kutowa maelezo kabla ya Utiaji wa Saini ya
Maelewano (MOU) kuhusu Mradi wa Ufuaji wa Umeme wa Nishati ya Gesi Zanzibar,
hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.
MUFTI Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi na
(kushoto) Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Fedha na Mipango Mhe.Jamal Kassim Ali na
(kulia) Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dr. Abdalla Juma Mabodi na
Mwananasheria Mkuu Dk. Mwinyi Talib Haji, wakifuatilia hatuba ya Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi
(hayupo pichani) akizungumza baada ya kumalizika kwa Utiaji wa Saini ya Maelewano
(MOU) Mpango Mkuu wa Upembuzi yakinifu juu ya Ujenzi wa Bandari Shirikishi ya
Uvuvi katika eneo la Mpiga Duri Unguja na Mkoani Pemba pamoja na Mradi wa
Ufuaji wa Umeme wa Nishati ya Gesi, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa
Ikulu Jijini Zanzibar.RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza wakati wa hafla ya utiaji wa
Saini ya Maelewano (MOU) Mpango Mkuu wa Upembuzi yakinifu juu ya ujenzi wa
Bandari Shirikishi ya Uvuvi katika eneo la Mpiga Duri na Mkoani Pemba na Mradi
wa Ufuaji wa Umeme wa Nishati ya Gesi Zanzibar, hafla hiyo imefanyika katika
ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar
BAADHI ya Viongozi wa Serikali wakifuatilia
hafla ya Utiaji wa Saini ya Maelewano (MOU) kuhusu Mpango Mkuu wa Upembuzi
yakinifu juu ya Ujenzi Bandari Shirikishi ya Uvuvi katika eneo la Mpiga Duri
Unguja na Mkoani Pemba na Mradi wa Ufuaji wa Umeme wa Nishati ya Gesi Zanzibar,
wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.
Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akizungumza katika hafla hiyo imefanyika
katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.
BAADHI ya Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama
Zanzibar wakifuatilia hafla ya Utiaji wa Saini ya Maelewano (MOU) kuhusu Mpango
Mkuu wa Upembuzi yakinifu juu ya Ujenzi wa Bandari Shirikishi ya Uvuvi katika eneo la Mpiga Duri Unguja na Mkoani
Pemba na Mradi wa Ufuaji wa Umeme wa Nishati ya Gesi Zanzibar. hafla hiyo
imefanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 3-2-2021
MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed
Suleiman Abdulla, Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe.Zuberi Ali Maulid, Jaji
Mkuu wa Zanzibar Mhe.Omar Othman Makungu na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na
Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Zena Ahmed Said.wamsikiliza Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani )
akihutubia katika hafla ya utiaji wa Saini ya Maelewano (MOU) Mpango Mkuu wa
Upembuzi yakinifu juu ya ujenzi wa Bandari Shirikishi ya Uvuvi katika eneo la
Mpiga Duri na Mkoani Pemba na Mradi wa Ufuaji wa Umeme wa Nishati ya Gesi
Zanzibar, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar
No comments:
Post a Comment