Na.Kassim Salum OMPR.
Mwenyekiti mwenza wa Kamati hiyo ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla alitoa kwa watanzania muda utakapowadia
kushiriki vyema katika zoezi la sense ya watu na makaazi bila ya kujali itikadi
zao za kisiasa, kidini, kikanda au tofauti yoyote ya kimaumbile.
Mhe. Hemed alisema
kushiriki katika zoezi la sense kwa wananchi ni jambo la msingi kwani takwimu
zinalisaidia taifa katika kupanga, kutathmini na kuratibu mipango ya maendeleo
ya nchi na kukosa kushiriki katika zoezi hili litawia vigumu kwa taifa kufikia
maendeleo jumuishi kwa maslahi mapana kwa watu wake.
Aidha, Makamu wa Pili
alieleza kuwa kuengezeka kwa utaalamu wa kuendesha zoezi la sense nchini ni
jambo la kujivunia kutokana na sense ya mwaka 2012 kuendeshwa na wataalamu
wazalendo ukilinganisha na sense zilizopita katika miaka ya nyuma.
Alifafanua kuwa, mbali
na ushiriki wa washirika wa maendeleo katika zoezi la sense nchini lakini ni
jambo jengine la kujivunia kuona Serikali ya Tanzania imekuwa ikichangia
asilimia kubwa katika kutekeleza zoezi hilo akitolewa mfano mwaka 2002 serikali
ilichangia gharama kwa asilimia 70, sense ya mwaka 2012 serikali ilichangia
gharama kwa asilimia 90, Na kwa sense ya mwaka 2022 serikali inakadiria
kuchangia asilimia 95 ya bajeti yote ya sense.
Alisema uchangiaji huo
wa bajeti unaashiria mwenendo mzuri namna serikali zote mbili zinavyothamini na
kutambua umuhimu wa takwimu zinazotokana na sense ya watu na makaazi.
Pia Makamu wa Pili wa
Rais alisema, Fanikio jengine kubwa Tanzania kwa kushirikiana na wadau
imefanikiwa kusomesha vijana wengi katika fani ya TAKWIMU na TEHAMA kwa kufikia
kiwango cha Uzamili na Uzamivu jambo linaloashiria zoezi la sense la 2022
litaendeshwa kwa uweledi wa hali ya juu.
“Tuna matarajio makubwa
sense ya 2022 itafanyika kwa ubora na weledi wa hali ya juu kabisa kutokana na
utalamu uliopo na teknolojia ya kisasa itakayotumika” Alisema Makamu wa Pili.
Pamoja na mambo
mengine, Makamu wa Pili alisema serikali ya awamu ya nane kama zilivyo awamu
nyengine zilizotangulia inathamini na kutambua umuhimu wa sense ya watu na
makaazi katika maendeleo ya watu wake, hivyo viongozi na wananchi wa Zanzibar
wako tayari kutekeleza zoezi hilo kwa lengo la kujenga mustkbali wa maendeleo
ya Zanzibar na wananchi wake.
“Napenda
niwathibitishie kwamba serikali ya mapinduzi Zanzibar inayongozwa na Rais wa
Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi imelipokea
zoezi hili la kitaifa na italisimamia na kulitekeleza kwa nguvu zake zote kwa
maslahi mapana ya wananchi tunaowaongoza”
Alieleza Mhe. Hemed.
Mhe. Hemed alisema
kutokana na sense kuwa katika mambo ya Muungano zoezi hilo litaanyika kwa
ushirikiano kati ya Ofisi mbili za takwimu akizitaja ile Ofisi ya Taifa ya
Takwimu (NBS) na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa serikali ya mapinduzi Zanzibar.
Wakiwasilisha taarifa za muelekeo wa sense ya mwaka 2022 Mtakwimu mkuu
kutokanza Ofisi ya Mtakwimu mkuu Zanzibar Bi Mayasa M. Mwinyi na Mtakwimu Mkuu
kutoka serikali ya Jamuhuri ya Muungano Dk. Albina Chuwa walisema sense ya 2022
itakuwa ya aina yake kutokana na mipango na mikakti mizuri iliowekwa kwa
kutumia teknolojia ya kisasa ambapo vijana wenye weledi na uzoefu wamekwisha
andaliwa.
Kutokana na matumizi
hayo ya Teknolojia yatapelekea matokeo ya sense hiyo kutolewa nmdani ya kipindi
cha muda mfupi huku ikizingatia vitegezo vya kimataifa.
Aidha, Wakuu hao wa
Taaisi hizi wamemuahidi Mhe. Waziri Mkuu na Makamu wa Pili wa Rais kuwa Taasisi
zao zimejipanga vyema kwa kuzingatia nguvukazi yay a kutosha walikuwa nayo.
Wakuu hao wa taaisi
hizo walieleza kuwa kutokana na serikali ya awamu ya sita ya jamuhuri ya
Muungano wa Tanzania na serikali ya awamu ya nane kutambua umuhimu wa sense
viongozi wake wameamua kutekeleza zoezi hili kwa vitendo kwa lengo la
utekelezaji wa ilani ya chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020-2025.
Walieleza kwamba sense
ya 2022 itakwenda kuzingatia na kutoa taarifa sahihi zinazohitajika kitakwimu
kupitia ngazi ya vijiji,kata, shihia hadi mitaa huku ikizingatia takwimu za
watu kielimu, kiafya na kiajira.
“Hakuna serikali yoyote
duniani inayopanga mipango yake ya kimaendeleo bila ya kuzingatia Takwimu za
watu wake Kielimu, Kiafya na Kiajira” Walieleza wakuu hao wa Taasisi.
Akitoa Salamu
kutoka shirika la umoja wa mataifa linaloshughulikia idadi ya watu na Makaazi
(UNFPA) Bi Jaqueline MahonAlisema shirika hilo litaendelea kutoa msaada kwa
serikali ya Jamuhuri ikiwemo vifaa, ramani pamoja na mahitaji mengine katika
kuhakikisha zoezi hilo linafanikiwa kama shirika hilo lilivyoshiriki katika
sense zilizotangulia.
Sensa ya watu na
makaazi nchini inafanyika kwa mujibu wa kifungu cha 6(2a) cha sheria ya takwimu
(Statistics Act) na kwa mujibu wa Katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania ya
mwaka 1977 ikiwa sense ni miongozi mwa masuala ya Muungano.
No comments:
Post a Comment