MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe.Othman Masoud
Othman akikabidhiwa Vifaa vya Maabara vya uchunguzi wa Covid 19, vilivotolewa
na Kampuni ya SD Biosensor ya Korea akikabidhiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa
Kampuni ya Vital Supplies Limited ya Tanzania Bw. Jimmy C Apson. hafla hiyo
imefanyika katika ukumbi wa Sheikh.Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar,
na (kushoto kwa Makamu) Waziri wa Afya,Ustawi wa Jamii,Wazee,Jinsia na Watoto
Zanzibar Mhe.Nassor Ahmed Mazrui na (kulia kwa Mkurugenzi) CEO wa Vital
Supplies Limited Bw.Sanjay Patadia wakipika makofi wakati wa hafla hiyo ya
makabidhiano.
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe.Othman Masoud
Othman akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Vital Supplies Limited
Bw. Jimmy C. Apson na CEO wa kampuni hiyo Bw. Sunjay.Patadia wakiwa na Viongozi
wa Wizara ya Afya,Ustawi wa Jamii,Wazee,Jinsia na Watoto Zanzibar,alipowasili
katika viwanja vya ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar
wakati wa hafla ya kukabidhiwa Vifaa vya Maabara vya Vipimo vya Uchunguzi wa
Covid 19, vilivyotolewana Kampuni ya SD.Biosensor ya Korea.
CEO wa Kampuni ya Vital Supplies Limited Tanzania
Bw.Sanjay Patadia akizungumza katika hafla ya kukabidhi Vifaa vya Maabara vya
Uchunguzi wa Covid 19 kwa Wizara ya Afya Zanzibar, vilivyotolewa na Kampuni ya
SD Biosensor kutoka Korea, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Sheikh Idrisa
Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar.
BAADHI ya Madaktari na Maofisa wa Wizara ya Afya
Zanzibar wakifutilia hafla ya kukabidhi Vifaa vya Maabara vya uchunguzi wa
Covid -19, vilivyotolewa na Kampuni ya SD Biosensor ya Korea, hafla hiyo
imefanyika katika ukumbiu wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini
Zanzibar.
KATIBU Mkuu Wizara ya Afya,Ustawi wa Jamii,Wazee
Jinsia na Watoto Zanzibar Dkt. Omar Dadi Shajak akizungumza na kutowa maelezo
ya makabidhiano ya Vifaa vya Maabara vya uchunguzi wa Covid 19, vilivyotolena
Kampuni ya SD Biosensor ya Korea, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Sheikh
Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar.
WAZIRI wa Afya,Ustawi wa Jamii,Wazee,Jinsia na Watoto
Zanzibar. Mhe Nassor Ahmed Mazrui, akizungumza katika hafla ya kukabidhiwa
Vifaa vya Maabara vya uchunguzi wa Covid 19, vilivyotolewa na Kampuni ya SD
Biosensor ya Korea kwa Wizara ya Afya,Ustawi wa Jamii,Wazee,Jinsia na
Watoto Zanzibar, hafla hiyo imefanyika
katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar.
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe.Othman Masoud
Othman akizungumza katika hafla ya kukabidhiwa Vifaa vya Maabara kwa ajili ya
Wizara ya Afya,Ustawi wa Jamii,Wazee,Jinsia na Watoto Zanzibar, vilivyotolewa
na Kampuni ya SD Biosensor ya Korea, kwa ajili ya uchunguzi wa Covid 19, hafla
hiyo imefanyika katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini
Zanzibar.
CEO wa Kampuni ya Vital Supplies Limited Bw.Sanjay
Patadia akimsikiliza Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe.Othman Masoud
Othman, akizungumza na kutowa shukrani kwa Kampuni ya SD.Biosensor ya Korea kwa
kutowa msaada huo wa Vifaa vya Maabara vya uchunguzi Covid 19,kwa Wizara ya
Afya,Ustawi wa Jamii,Wazee,Jinsia na Watoto Zanzibar, hafla hiyo imefanyika
katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar.
Na Miza Kona Maeleao Zanzibar 21/05/2021
Makamu wa Kwanza wa Rais Mhe.Othman Masoud Othman ameitaka jamii kufuata miongozo ya afya na kuongeza hamasa ya mapambano ili kujikinga ugonjwa wa Corona nchini.
Makamu wa Kwanza ameyasema huko katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Mjini Zanzibar katika hafla Makabiadhiano ya Vifaa vya haraka vya kupimia Virusi vya Corona, amesema ni jukumu la kila mtu kuongeza kasi ya mapambano dhidi ya ugonjwa huo .
Amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania inachukua jitihada kubwa ya kupambana na ugonjwa Corona nchini, vifaa hivyo vitasaidia kuongeza kasi ya kiwango cha upimaji wa virusi vya ugonjwa huo katika jamii.
Amefahamisha ugonjwa wa Corona umeathiri kwa kiasi kikubwa duniani hivyo ni vyema kushirikiana wafadhili na wadau mbalimbali katika kujenga miundombinu mizuri ya afya ili kuepukana na maambukizi.
Makamu wa Kwanza amewasisita wafanyakazi wa wizara ya afya kuitumia vyema msaada huo kwa kufikia malengo yaliyokusudiwa.
Akizungumzia kuhusu hali ya maambukizi nchini Makamu wa kwanza amesema kuwa ugonjwa upo lakini hali sio mbaya hivyo amewasisitiza wananchi kuwa watulivu na kutosikiliza taarifa potofu zinazotolewa katika mitandao ya kijamii ili kuepuka taharuki.
Nae Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto mhe. NassorAhme Mazrui amesema ugonjwa Corona ni tishio duniani ni vyema jamii kufuata maelekezo yanayotolewa na wataalamu wa afya ili kujikinga na maambukizi .
Amefahamisha kuwa vifaa hivyo vya kupimia virusi vya Corona ni vyenye ubora wa hali ya juu ambavyo hutoa majibu ya papo kwa papo vitasaidia kugundua kwa haraka wale wenye kupata maambukizi ya ugonjwa huo.
Mapema Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Supplier CEO Sunjay C. Patadia amesema kampuni yake ina uwezo wa kutengeneza dawa na vitendakazi vyevye ubora kimataifa na vifa vipo tayari kwa ajili ya kutoa huduma kwa jamii bila madhara.
Vifaa hivyo vya haraka vya kupimia Virusi vya Corona vyenye thamani ya Tsh. Milioni 250 vimetolewa na Kampuni ya SD BIOSENSOR na SUPLIER CEO kutoka Korea
No comments:
Post a Comment