Na Jaala Makame Haji - ZEC
Tume
ya Uchaguzi ya Zanzibar ZEC imezitaka Taasisi zilizozoshiriki kuangalia
Uchaguzi Mkuu kuwasilisha ripoti zao za uangalizi kwa kutoa mapendekezo yenye
nia ya kujenga Amani na utulivu na kutanguliza maslahi ya wananchi kuliko kueleza zaidi hisia
za kisiasa
Ushauri
huo ulitolewa na Makamo Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar Mhe. Mabruki
Jabu Makame katika Ukumbi wa Mikutano wa Tume hiyo Maisara Zanzibar mara baada
ya kupokea ripoti ya waangalizi wa Uchaguzi Mkuu 2020 kutoka Jumuiya ya
kupambana na Changamoto za Vijana Zanzibar ZAFAYCO
Makamo
Mwenyekiti huyo alisisitiza kuwa Changamoto na Mapendekezo yaliyowasilishwa
katika ripoti za uangalizi zina lengo la kumarisha uendeshaji na Usimamizi wa
Chaguzi zijazo
Hata
hivyo, ZEC imezipongeza Taasisi za ndani ya nchi zilizoshiriki kuangalia
Uchaguzi Mkuu 2020 kwa kuwa wa Mwanzo kutoa matamko juu ya mwenendo wa Uchaguzi
kuliko taasisi za nje ya nchi hali ambayo ni tofauti na chaguzi zilizopita.
Kwa
upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Jumuiya ya ZAFAYCO Abdalla Ali Abeid
alieleza kuridhishwa kwake na utendaji wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar katika
kuendesha na kusimamia Uchaguzi Mkuu 2020 kwa vile Tume hiyo iliyashirikisha
kwa karibu zaidi makundi ya Vijana kushiriki katika harakati za Uchaguzi.
Ndugu
Abdallah alieleza kuwa, ZAFAYCO iliridhishwa na uamuzi wa ZEC wa kuondosha
ukomo wa idadi ya Waangalizi kwa taasisi za Uangalizi wa Uchaguzi Mkuu 2020
hali ambayo iliufanya Uchaguzi Mkuu 2020 kuwa huru na wazi katika hatua zote
kuanzia Uandikishaji hadi upigaji kura
Taasisi
ya kupambana na changamoto za Vijana Zanzibar ZAFAYCO imewasilisha Tume ya
Uchaguzi ya Zanzibar ripoti ya Uangalizi wa Uchaguzi Mkuu 2020 uliofanywa na
Waangalizi kutoka Taasisi hiyo.
No comments:
Post a Comment