Habari za Punde

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. Philip Isdor Mpango Awasilisha Ahadi za Tanzania Katika Jukwaa la Usawa Paris Nchini Ufaransa.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika linaloshughulikia masula ya wanwake UN WOMEN Dkt. Phumzile Mlambo Ngcuka mara baada ya Makamu wa Rais kumaliza kuwasilisha ahadi za Tanzania katika Jukwaa la Kizazi Chenye Usawa- Paris Ufaransa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika linaloshughulikia masula ya wanwake UN WOMEN Dkt. Phumzile Mlambo Ngcuka mara baada ya Makamu wa Rais kumaliza kuwasilisha ahadi za Tanzania katika Jukwaa la Kizazi Chenye Usawa- Paris Ufaransa.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango akiwasilisha ahadi za Tanzania katika kulinda haki za Kiuchumi za wanawake katika Jukwaa la Kizazi Chenye Usawa - Paris Ufaransa
 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango ametaja hatua zitakazochukulia na Tanzania katika kuboresha haki za kiuchumi kwa wanawake.

Makamu wa Rais ameyasema hayo katika Jukwaa la Kizazi Chenye Usawa (Generation Equality Forum) linalofanyika Paris Ufaransa.

Kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais amesema Tanzania inachukua hatua muhimu ili kukuza na kulinda  haki za kiuchumi kwa wanawake.

Mheshimiwa Makamu wa Rais amezitaja hatua hizo ni pamoja nakuongeza vituo vya kulea watoto mchana katika maeneo mbalimbali ya shughuli za kiuchumi kama vile sokoni na maeneo mengine ya kazi .

Makamu wa Rais amesema serikali inachukua hatua za kuongeza upatikanaji wa huduma muhimu za kijamii kama vile umeme, maji pamoja na nishati mbadala ili kuwapunguzia wanawake mzigo wa majukumu mengi katika maeneo ya vijijini na baadhi ya mjini.

Aidha amesema serikali itaongeza upatikanaji wa teknolojia rahisi na sahihi ili kuongeza tija na ufanisi katika shughuli zinzazofanywa na wanawake katika  uzalishali mali.

Makamu wa Rais amesema hatua nyingine ni pamoja na kuongeza fursa za elimu kwa wanawake ikiwemo kuanzisha shule za sayansi kwa wasichana, elimuya ufundi stadiili kuwapatia ujuzi na stadi zinazowezesha kuzalisha kwa tija.

Hatua nyingine ni pamoja na kuwawezesha wanawake kumudu na kutumia teknolojia za kidijitali kwaajili ya kuongeza ushindani katika uzalishaji na shughuli zao mbalimbali za kiuchumi.

Kuwawezesha wanawake kupata afua za kifedha kwa kutumia ubunifu wa aina mbalimbali ikiwemo kutumia njia za kielektroniki.

Kuondoa fikra na tamaduni potofu zinazozuia wanawake kujihusisha na shughuli za kiuchumi ikiwemo umiliki wa ardhi.

Kupanua wigo wa huduma za hifadhi ya jamii ili kujumuisha kaya ambazo zipo nje ya uchumi rasmi.

Urasimishaji wa biashara zenye staha zinazofanywa na wanawake ili kuweza kupata huduma za kifedha.

Kuimaraisha mifuko ya uwezeshaji wanawake kiuchumi ili kurahisisha kupata mitaji ya kuanzisha shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Mara baada ya kuwasilisha ahadi hizo, Makamu wa Rais amekutana na kufanya mazungumzo na Dkt.  Phumzile Mlambo Ngcuka Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masuala ya wanawake (Un- Women)

Dkt Phumzile amesema amefurahishwa na ahadi zilizotolewa na serikali ya Tanzania katika kuchagiza haki za kiuchumi za wanawake na kumpongeza makamu wa Rais kwa uwakilishi mzuri.  Makamu wa Rais amemuhakikishia Dkt Phumzile kwamba Tanzania itaendelea kusimamia na kulinda haki za kiuchumi za wanawake.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.