Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Faustine Ndugulile (mwenye barakoa nyeusi) akimpokea Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa alipowasili kuzindua Huduma Pamoja kwenye viwanja vya Posta, Dar es Salaam.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipozindua Mradi wa Vituo vya Huduma Pamoja (One Stop Centre) kupitia Shirika la Posta Tanzania kwenye viwanja vya Posta Makao Makuu jijini Dar es salaam,
Na Beatrice Sanga, MAELEZO, Dar. Septemba 06, 2021. WAZIRI Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa amezitaka Taasisi za Serikali zinazotoa huduma kwa wananchi, ambazo hazijajiunga na utaratibu wa Vituo Huduma pamoja vilivyopo kwenye Shirika la Posta Tanzania, kujiunga na huduma hiyo ndani ya mwaka huu wa 2021-2022 ili kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Amesema ilani ya
chama cha Mapinduzi ya 2020 inaelekeza serikali kurahisisha utoaji wa huduma
mbalimbali kwa umma, kwa kuanzisha vituo vya huduma ya pamoja ili kuongeza
ufanisi ambapo mradi wa huduma hiyo iliyopo Posta ni sehemu ya utekelezaji wa
mradi wa kitaifa wa ‘Tanzania ya kidijitali’ na kuzitaja Taasisi na Wizara ambazo
zinatakiwa kujiunga na huduma hiyo kuwa ni pamoja na Wizara ya Ardhi, Wizara ya
Utumishi (Tume ya Ajira), TIC, TMDA, NEMC, EPZA na TBS.
Ameyasema hayo
Septemba 06 2021 alipokuwa akizindua rasmi mradi wa vituo vya Huduma Pamoja wa Shirika
la Posta Tanzania, Hafla iliyofanyika katika viwanja vya makao makuu ya shirika
hilo Jijini Dar es Salaam ambapo vituo vya huduma pamoja vilivyozinduliwa ni Idara ya Uhamiaji , Mamlaka ya Mapato
Tanzania(TRA), Wakala ya Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Mamlaka ya
Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhaminia (RITA),
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa
Watumishi wa Umma (PSSSF)
"Nazielekeza
taasisi zote zinazotoa huduma kuongeza kasi ya kujiunga na utaratibu wa huduma pamoja
taasisi ambazo hazijaanza kutoa huduma sasa zijipange kuhakikisha kuwa zinatoa
huduma katika vituo hivi ndani ya mwaka huu 2021- 2022” Amesema
Mhe. Majaliwa
Kwa upande wake
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dk. Faustine Ndungulile
ameishukuru serikali ya awamu ya sita ambayo ilianza kuja na mradi wa vituo vya
huduma pamoja, ili kuwarahisishia wananchi kupata huduma kwa urahisi na haraka.
Dkt. Ndugulile
amesema vituo hivi vina lengo la kuweka pamoja watoa huduma na wateja wao, ili
kurahisisha huduma za serikali ambapo
mpaka sasa, serikali imetoa fedha za awali
Sh Bilioni 3.9 na fedha hizo zitaelekezwa katika dijitali posta (digital
postal) pamoja na kununua nyenzo zitakazorahisisha usafirishaji kupitia posta
na kuahidi kufanya mabadiriko makubwa ndani ya shirika lengo likiwa ni kuifanya
posta, kuwa posta ya kidijitali.
“sisi
kama wizara tumezamiria kwamba tunafanya mabadiliko makubwa sana ndani ya
shirika letu la posta na mimi kama Waziri nina ridhika na hatua za awali na
mafanikio ambayo yamefikiwa na shirika letu la posta. tumedhamiria kuhakikisha
kwamba posta yetu inakwenda kuwa posta ya kidigitali”
Amesema Dkt. Ndungulile
Naye Kaimu Posta Masta Mkuu Bw. Macrice Mbodo, ameeleza
kuwa, utekelezaji wa mradi wa huduma ya pamoja utatekelezwa kwa awamu tatu,
ambapo awamu ya kwanza ya utekelezaji wa
mradi huu utafanyika kwa kipindi cha
miezi 18 kilichoanza Mwezi Julai 2021 mpaka Desemba 2022 ampapo katika awamu hii, huduma za serikali
zitatolewa kwa wananchi katika mtindo wa
huduma moja dirisha moja(multiple window system), na kila dirisha litakuwa linahudumia
mwananchi katika dirisha lake, ambapo vituo kumi , vinatarajiwa kufunguliwa vikiwemo
vituo vya Dodoma, Arusha, Mbeya, Mwanza, Tanga Kigoma, Unguja na Pemba
Ameendelea kueleza kuwa, katika
awamu ya pili vituo kumi na saba vinatarajiwa kufunguliwa ambavyo vitahusisha
vituo vya Pwani Iringa Rukwa Ruvuma, Kilimanjaro, Tabora, Mara, Lindi, Mtwara, Manyara,
Katavi, Njombe na Geita.
Aidha,kipindi cha awamu ya tatu ya mradi huu utahusisha kipindi cha miezi 18 Julai-Disemba (Single Window System) itakayoanza Julia 2024 dec 2025 katika awamu hii huduma za serikali zitaanza kutolewa katika mtindo wa dirisha moja huduma zote ( single window system )ambapo vituo vitafunguliwa katika Wilaya zote za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
No comments:
Post a Comment