Waziri wa Afya , Ustawi wajamii ,Wazee, Jinsia na Watoto Nassor Ahmed Mazrui (kushoto) akimkabidhi Meneja wa masoko ya Kimataifa hospital ya PUSHPAWATI iliopo Nchini India Sanoj Kumar (katikati) kitabu cha kumbukumbu ya Zanzibar mara walipofika ofisini kwake kujitambulisha, wamwanzo kulia ni Mjumbe kutoka Hospitali hiyo Ratnesh Sinha.
Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii Wazee
Jinsia na Watoto, Nassor Ahmed Mazrui amesema wizara yake inatarajia
kushirikiana na Hospitali ya Pushpawati
singhania ilioko Delhi nchini india katika kuwapatia matibabu bora wananchi wa Zanzibar.
Alisema hayo ofisini kwake Mnazi
Mmoja Mjini Unguja, wakati alipokutana na uongozi wa Hospitali hiyo uliofika wizarani
hapo kwa ajili ya kujitambulisha.
Alisema hospitali hiyo itasaidia
katika kuwapatia wananchi huduma mbalimbali za matibabu ikiwemo moyo, matatizo
ya haja ndogo pamoja na upandikizaji wa
figo.
Alieleza kuwa, hospitali hiyo
imeamuwa kwa makusudi kushirikiana na Zanzibar katika huduma za afya ili kuwasaidia madaktari wa Zanzibar waweze kupata
ujuzi na uzoefu wa kutumia mashine za kisasa na kufanya uchunguzi wa maradhi mbalimbali ya
binadamu.
Aidha alisema, hatua inayofuata ni
kuandaa taratibu za kusaini hati ya makubaliano baina ya Wizara hiyo na Hospitali
ya Pushpawati kwa lengo la kuanza kusaidia huduma za matibabu nchini.
Nae Meneja wa Masoko ya Kimataifa wa
Hospitali hiyo, Sanoj Kumar amesema ipo haja
ya kuwaleta wataalamu wao Zanzibar ili kusaidia utoaji wa huduma za
matibabu kwa wananchi.
Alisema ushirikiano huo pia utasaidia
katika kupunguza gharama za matibabu kwa wagonjwa wanaokwenda nchini india kwa
ajili ya matibabau.
Aidha alisema Hospitali ya Pushpawati
singhania, itaendelea kushirikiana kwa karibu na serikali ili kuhakikisha huduma bora za afya
zinapatikana Zanzibar.
No comments:
Post a Comment