Habari za Punde

Rais Dk Hussein Mwinyi atuma salamu za rambirambi kwa familia kufuatia kula kasa anayesadikiwa kuwa na sumu

 

STATE HOUSE ZANZIBAR

OFFICE OF THE PRESS SECRETARY

PRESS RELEASE

Zanzibar                                                                                       26.12.2021

---

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ametoa salamu za rambirambi kwa familia za marehemu waliofariki kufuatia kula samaki wa aina ya kasa anayesadikiwa kuwa na sumu huko Matemwe, Mkoa wa Kaskazini Unguja.

 

Katika salamu hizo za rambirambi, Rais Dk. Mwinyi ameeleza kusikitishwa na vifo hivyo na kuzinasihi familia za marehemu hao kuwa na subira na ustahamilivu katika kipindi hichi kigumu cha msiba pamoja na kumuomba Mwenyezi Mungu kuwaponya kwa haraka waliodhurika baada ya kula samaki huyo.

 

Rais Dk. Mwinyi katika salamu hizo za rambirambi, amesema kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara yake husika itaendelea kuhakikisha wale wote waliodhurika wanaendelea kupatiwa tiba ili waweze kurudi katika hali zao nzuri za kiafya.

 

Imetayarishwa na Kitengo cha Habari

Ikulu Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.