Katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Rais Dk. Mwinyi aliagwa na viongozi mbali mbali wakiongozwa na Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdullah ambapo baada ya kuwasili kisiwani humo akiwa amefuatana na mkewe Mama Mariam Mwinyi alipokewa na viongozi mbali mbali wa vyama vya siasa na Serikali wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Matar Zahor Masoud.
Akiwa kisiwani Pemba, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Mwinyi hapo kesho (Januari 03.2022) mapema asubuhi anatarajiwa kushiriki katika ufunguzi wa Matembezi ya Vijana wa UVCCM Zanzibar huko Konde, Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Aidha, Rais Dk. Mwinyi baada ya shughuli hiyo anatarajiwa kuwasili Kinyasini Wete kwa ajili ya kuweka jiwe la Msingi Kiwanda cha kutengeneza Maji Safi Watercom (T) Ltd na baadae kuwahutubia wananchi.
Imetayarishwa na Kitengo cha Habari,
No comments:
Post a Comment