RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu (ZAWA) Dkt. Salha Mohamed Kassim, akitowa maelezo ya Kitaalamu ya ujenzi wa Matangi ya Maji Safi na Salama Kwarara Kidutani, wakati wa hafla ya uwekaji wa Jiwe la Msingi la Mradi wa Uhuishaji na Uimarishaji wa Mfumo wa Usambazaji Maji Zanzibar, ikiwa ni Wiki ya Maji Duniani.(kulia kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe.Idrisa Mustafa Kitwana na (kushoto kwa Rais) Waziri wa Maji Nishati na Madini Mhe. Shaib Kaduara.(Picha na Ikulu)
WAFANYAKAZI wa Kampuni ya L&T Construction wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akihutubia katika hafla hiyo ya uwekaji wa Jiwe la Msingi la Mradi wa Uhuishaji na Uimarishaji wa Mfumo wa Usambazaji wa Maji Zanzibar, hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya ujenzi matangi ya maji ya mradi huo Kwarara Kidutani Wilaya ya Magharibi “B”Unguja.(Picha na Ikulu)
WANANCHI wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja wakifuatilia hutuba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akihutubia wakati wa hafla ya uwekaji wa Jiwe la Msingi la Mradi wa Uhuishaji na Uimarishaji wa Mfumo wa Usambazaji wa Maji Zanzibar.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.,Hussein Ali Mwinyi akihutubia katika hafla ya Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Mradi wa Uhuishaji na Uimarishaji wa Mfumo wa Usambazaji Maji Zanzibar, hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya ujenzi wa matangi ya maji ya Mradi huo Kwarara Kidutani Wilaya ya Magharini “B” Unguja ikiwa sambamba na maadhimisho ya Wiki ya Maji Duniani.(Picha na Ikulu)
/RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikabidhiwa zawadi maalum na Mwakilishi wa Kampuni ya L&T Construction Bw.Hari Prakash, (kushoto kwa Rais) baada ya kumalizika kwa hafla ya Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Mradi wa Uhuishaji na Uimarishaji wa Mfumo wa Usambazaji wa Maji Zanzibar, mradi huo wa ujenzi wa matangi ya maji katika eneo la Kwarara Kidutani Wilaya ya Magharibi “B” Unguja.(Picha na Ikulu)
No comments:
Post a Comment