Habari za Punde

WAZIRI DKT. GWAJIMA ATOA MREJESHO MIKUTANO YA KIMATAIFA

 Na WMJJWM- Dodoma

 

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt Dorothy Gwajima ametoa mrejesho wa mikutano miwili ya Kimataifa aliyoshiriki  ikiwemo Mkutano wa 66 wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu hali za Wanawake Duniani uliofanyika nchini Marekani na ule wa Mkutano wa G7 Care Work uliofanyika nchini Ujerumani.

 

Dkt. Gwajima akizungumza na wadau mbalimbali wa masuala ya Wanawake na Jinsia jijini Dodoma alisema Tanzania ikishiriki mikutano hiyo kwa lengo la kwenda kujifunza na kueleza Duniani nini Tanzania inafanya katika kuwawezesha wanawake kiuchumi na Usawa wa Kijinsia.

 

"Mimi binafsi nilialikwa na nilishiriki katika mkutano huo ambapo niliambatana na mtaalamu mmoja. Mkutano huo ni muhimu sana kwa kuwa kama mnavyofahamu Mhe. Mama Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye aliahidi kuwa kinara wa utekelezaji wa eneo la Pili kuhusu Haki na Usawa wa Kiuchumi kwenye Jukwaa la usawa wa Jinsia" alisema Dkt. Gwajima

 

Aidha Dkt. Gwajima amesema lengo la Mikutano hiyo muhimu ni kujadli masuala mbalimbali ya maendeleo ya wanawake ikiwa ni pamoja na mafanikio na changamoto zilizopo zipate maamuzi ya kisera na kiutekelezaji kutoka kwa viongozi na wataalam.

 

"Nimeitisha kikao hiki ili nitoe mrejesho wa mikutano hiyo miwili na pia kuweka mikakati ya utekelezaji wa maazimio ya mikutano hiyo na kupitia kikao hiki pia nitaomba tujipange vizuri zaidi ili kuwa na ushiriki bora zaidi katika mikutano hii kwa wakati mwingine" alisisitiza Dkt. Gwajima

 

 

Pia Dkt. Gwajima amewashukuru wadau waliowezesha ushiriki wa Tanzania katika Mkutano wa 66 wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu hali za Wanawake Duniani na ule wa Mkutano wa G7 Care Work ambao ni UN Women, UNFPA, Ubalozi wa Ireland na Asasi ya LSF, LANDESA na OXFAM ambazo zilichangia katika kuwezesha Viongozi na wataalam kushiriki mikutano hiyo.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima, akifungua kikao cha tathmini ya Mkutano wa 66 wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu hali za Wanawake Duniani na Mkutano wa G7, Mikutano ambayo Mhe. Waziri alihudhuria akiwa na wataalam wa Tanzania kwa Nyakati Tofauti nchini Marekani na Ujerumani. 

Baadhi ya Wawakilishi kutoka Wizara, Taasisi, Mashirika Yasiyo ya Kiserikali na wadau wengine wakiwa katika kikao cha Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima alipotoa tathmini ya Mkutano wa 66 wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu hali za Wanawake Duniani na Mkutano wa G7 katika kikao kilichofanyika jijini Dodoma. 

Na WMJJWM- Dodoma

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt Dorothy Gwajima ametoa mrejesho wa mikutano miwili ya Kimataifa aliyoshiriki  ikiwemo Mkutano wa 66 wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu hali za Wanawake Duniani uliofanyika nchini Marekani na ule wa Mkutano wa G7 Care Work uliofanyika nchini Ujerumani.

 

Dkt. Gwajima akizungumza na wadau mbalimbali wa masuala ya Wanawake na Jinsia jijini Dodoma alisema Tanzania ikishiriki mikutano hiyo kwa lengo la kwenda kujifunza na kueleza Duniani nini Tanzania inafanya katika kuwawezesha wanawake kiuchumi na Usawa wa Kijinsia.

 

"Mimi binafsi nilialikwa na nilishiriki katika mkutano huo ambapo niliambatana na mtaalamu mmoja. Mkutano huo ni muhimu sana kwa kuwa kama mnavyofahamu Mhe. Mama Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye aliahidi kuwa kinara wa utekelezaji wa eneo la Pili kuhusu Haki na Usawa wa Kiuchumi kwenye Jukwaa la usawa wa Jinsia" alisema Dkt. Gwajima

 

Aidha Dkt. Gwajima amesema lengo la Mikutano hiyo muhimu ni kujadli masuala mbalimbali ya maendeleo ya wanawake ikiwa ni pamoja na mafanikio na changamoto zilizopo zipate maamuzi ya kisera na kiutekelezaji kutoka kwa viongozi na wataalam.

 

"Nimeitisha kikao hiki ili nitoe mrejesho wa mikutano hiyo miwili na pia kuweka mikakati ya utekelezaji wa maazimio ya mikutano hiyo na kupitia kikao hiki pia nitaomba tujipange vizuri zaidi ili kuwa na ushiriki bora zaidi katika mikutano hii kwa wakati mwingine" alisisitiza Dkt. Gwajima

  

Pia Dkt. Gwajima amewashukuru wadau waliowezesha ushiriki wa Tanzania katika Mkutano wa 66 wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu hali za Wanawake Duniani na ule wa Mkutano wa G7 Care Work ambao ni UN Women, UNFPA, Ubalozi wa Ireland na Asasi ya LSF, LANDESA na OXFAM ambazo zilichangia katika kuwezesha Viongozi na wataalam kushiriki mikutano hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Anthony Mtaka akizungumza katika kikao cha Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima, alipotoa tathmini ya Mkutano wa 66 wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu hali za Wanawake Duniani na Mkutano wa G7 katika kikao kilichofanyika jijini Dodoma. 

Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt Zainab Chaula akitoa maelezo ya awali katika kikao cha Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima alipotoa tathmini ya Mkutano wa 66 wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu hali za Wanawake Duniani na Mkutano wa G7 katika kikao kilichofanyika jijini Dodoma.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.