Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na
Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akitoa maelekezo wakati alipofanya ziara ya
kutembelea na kukagua ujenzi wa skimu ya umwagiliaji Kijiji cha Lukenge
wilayani Mvomero mkoani Morogoro unaotekelezwa na Ofisi ya Makamu wa Rais
kupitia Mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi kwa kutumia Mifumo Ikolojia
Vijijini (EBARR).
Waziri Jafo atoa maelekezo utekelezaji wa ujenzi wa
skimu ya umwagiliaji Mvomero
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na
Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo ameelekeza Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro
kuunda timu kukagua kusuasua kwa ujenzi wa skimu ya umwagiliaji katika Kijiji
cha Lukenge wilayani Mvomero na kuwasilisha taarifa ndani ya mwezi mmoja.
Amechukua hatua hiyo tarehe 17 Juni, 2022 wakati alipofanya
ziara ya kushtukiza kwa ajili ya kutembelea na kukagua Mradi wa Kuhimili Mabadiliko
ya Tabianchi kwa kutumia Mifumo Ikolojia Vijijini (EBARR) unaotekelezwa na Ofisi
ya Makamu wa Rais.
Dk. Jafo alionesha kushangazwa na hali aliyoikuta katika
mradi huo unaosimamiwa na wataalamu kutoka Wilaya ya Mvomero wakati Serikali
ilishatoa fedha zote ili utekelezaji huo ufanyike kwa wakati kama ilivyopangwa.
“Nimekuja kuangalia value
for money, sijaridhika na mradi huu wataalamu wametuingiza chaka hatuwezi
kuvumulia wataalamu wachache wanaotuvuruga, kwa hiyo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na
ndani yake wakiwemo TAKUKURU wachunguze mradi huu, tunataka kuona mradi huu
unakamilika kwa wakati tufanye kazi kwa maslahi ya wananchi,” alisema.
Hata hivyo, kwa upande wake Mratibu wa Mradi wa EBARR wilayani
humo, Bw. alisema mradi huo ulianza kujengwa mwaka 2013/14 umekaa kwa zaidi ya tisa
bila kuendelezwa hivyo waliwasilisha ombi Ofisi ya Makamu wa Rais ambayo
ilikubali kutoa fedha kiasi cha sh. milioni 710.
Alisema baada ya kupata fedha Mkurugenzi wa Wilaya
alituma wataalamu wakague eneo hilo walibaini changamoto liko chini mita moja
ukilinganisha na usawa wa mashamba usawa
“Wananchi wana kiu kuona mradi huu ukikamilika kwa
wakati ili uwasaidie kupata majawabu ya mustakabali wa maisha yao sasa hapa
tunataka mradi huu iwe mvua iwe jua tutaka uanze kufanya kazi,” alisisitiza.
Aliitaka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ijipange kununua
pampu ya kusukuma maji kwa kuwa wao ndio wasanifu wa mradi huo ili uweze kuanza
kufanya kazi kama ilivyotarajiwa.
Katika hatua nyingine Waziri Jafo alitembelea na kukagua
maendeleo ya ujenzi wa kisima cha maji safi katika Kijiji cha Mingo wilayani
humo ambapo alioneshwa kuridhishwa na utekelezaji wake.
Alitoa maelekezo kwa wataalamu kutoka Wakala wa Maji Mijini
na Vijijini (RUWASA) kukamilisha mradi huo Juni 28, 2022 kama walivyomuahidi
ili uweze kusaidia wananchi katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya
tabianchi.
“Nataka nione maji yanatiririka hapa na kwenda kwa wananchi
itakapofika asubuhi ya tarehe 29 mwezi Juni, tunataka kuona wananchi
wanafaidika na miradi hii ya mabadiliko ya tabianchi inayosimamiwa na Ofisi ya
Makamu wa Rais,” alisema.
Akiishukuru Serikali kwa niaba ya wananchi, Mwenyekiti
wa Kijiji cha Mingo, Bw. Rashid Kibukila aliishukuru Serikali kupitia Ofisi ya
Makamu wa Rais kwa kuwapelekea mradi huo.
Mbali ya Mvomero, mradi wa EBARR pia unatekelezwa katika halmashauri za wilaya za Mpwapwa (Dodoma), Kishapu (Shinyanga), Simanjiro (Manyara) na Kaskazini ‘A’ (Unguja).
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akikagua ujenzi wa tangi la majisafi katika Mingo wilayani Mvomero mkoani Morogoro unaotekelezwa na Ofisi ya Makamu wa Rais kupitia Mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi kwa kutumia Mifumo Ikolojia Vijijini (EBARR).
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akisaini kitabu alipowasili wilayani Mvomero mkoani Morogoro kwa ajili ya ziara ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa Mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi kwa kutumia Mifumo Ikolojia Vijijini (EBARR).
Sehemu ya mfereji wa skimu ya umwagiliaji Kijiji cha Lukenge wilayani Mvomero unaojengwa kupitia Mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi kwa kutumia Mifumo Ikolojia Vijijini (EBARR) ambao Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo aliukagua na kutoa maelekezo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na
Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akisikiliza maelezo kuhusu ujenzi wa skimu
ya umwagiliaji Kijiji cha Lukenge wilayani Mvomero mkoani Morogoro
unaotekelezwa kupitia Mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi kwa kutumia
Mifumo Ikolojia Vijijini (EBARR).
No comments:
Post a Comment