Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis leo tarehe 19 Juni, 2022 ametembelea na kukagua zoezi la upandaji miti katika maeneo mbalimbali jijini Dodoma.
Akikagua zoezi hilo katika
Barabara ya Ihumwa – Iyumbu, Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Medeli, Hospitali ya
Benjamin Mkapa na Iyumbu, Mhe. Khamis ameonesha kuridhishwa na usimamizi na
ufuatiliaji wa miti hiyo tangu ilipopandwa.
Alitoa pongezi kwa Wakala wa
Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Jiji la Dodoma, Wakala wa Barabara Tanzania
(Tanroads) na wadau mbalimbali wanaotoa mchango katika utunzaji wa miti.
“Leo tumefanya ziara ya
kukagua miti ambayo imepandwa kwasababu kuu mbili moja ni Sera yetu ya
Mazingira inatuelekeza tupande miti na kuiendeleza ili tujue ipi imeota na ipi
imekufa, lakini pia tunafanya ziara hii kufuatia maelekezo ya Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhhe. Dkt. Philip Mpango ambaye kwa nayakati mbalimbali
amekuwa akitusisitiza kufuatilia miti inayopanadwa,” alisema.
Aidha, Naibu Waziri Khamis
alitoa wito kwa wadau mbalimbali wa mazingira kuwa na ushirikiano katika kuhakikisha
miti inaoteshwa na kutunza ili kutimiza azma ya kuhakikisha mazingira
yanahifadhiwa na hivyo kuifanya Dodoma kuwa ya kijani.
Pia aliwasihi Tanroads wawe
wanawafuatilia watu waliowapa zabuni ya kumwagilia miti kuwa wafuatilie zoezi hilo
kama linafanyika kwa mujibu wa utaratibu uliopangwa.
Kwa upande wake Meneja
Msaidizi wa Maendeleo ya Rasilimali Misitu kutoka TFS, Bi. Patricia Manonga alisema
Programu ya Dodoma ya Kijani wanatarajia kuongeza uzalishaji wa miche kutoka
milioni moja hadi milioni mbili kwa mwaka kupitia kitalu kilichopo Mailimbili.
Alisema hadi kufikia sasa
tayari TFS imezalisha miche zaidi ya milioni 57 ambayo imepandwa katika maeneo
mbalimbali ya Mkoa wa Dodoma ambapo zoezi rasmi lilizinduliwa mwaka 2017.
Akitoa mchanganuo wa miti
iliyopandwa, Bi. Patricia alifafanua kuwa katika eneo la Medeli ilipandwa miti 500,
Iseni miti 1,200 na Iyumbu ilipandwa miti ya kivuli takriban 1,000 ambapo
amezitaka taasisi kupanda miche wanayopatiwa badala ya kuiacha ikaharibika.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis akikagua miti katika eneo la Medeli wakati wa ziara ya kukagua zoezi la upandaji miti jijini Dodoma leo tarehe 19, Juni 2022.
(PICHA NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS)
No comments:
Post a Comment