Habari za Punde

Mageuzi Makubwa ya Kilimo Ndio Yatakayowainua Wananchi wa Kibakwe.

 


Na mwandishi wetu.

Waziri wa Nchi Ofisi ya waziri mkuu, Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene amehimiza watendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mpwapwa kufanya mageuzi makubwa ya kilimo kwa kuwekeza katika miradi ya kimkakati iltakayoongeza uzalishaji katika sekta ya kilimo.

“Lazima tuwekeze fedha kwenye miundo mbinu ya uzalishaji wa kilimo, wataalam wa kilimo wanaojengewa uwezo na wizara ya kilimo, wafanye kilimo shambani nawatumie maarifa waliyopata kwa kushirikisha wakulima”

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu (Mb) Mhe. George simbachawene wakati alipofanya mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Kinusi Jimbo la Kibakwe katika Halmashauri ya wilaya ya Mpwapwa.

“Kata ya Malolo na kata Ipera ni eneo ambalo limejikita katika kilimo cha umwagiliaji, Halmashauri itizame namna ya kuimarisha miundo mbinu ya maji ili maji yasipote alisema Waziri”

Serikali ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan, katika bajeti yake ya 2022-2023 imejikita katika maeneo ya uzalishaji, bajeti ya kilimo imeongezwa kutoka billion 200 mpaka billion 900, hivyo fedha nyingi zitaletwa kijijini katika miradi ya kimkakati ya kilimo.

“Amefafanua serikali imeleta pembejeo za ruzuku, baadhi ya gharama zitalipwa na serikali ili mwananchi wapate pembejeo kwa bei nafuu ni lazima maafisa kilimo wajue hiyo mifumo ili waweze kuwasaidia wakulima”

Awali diwani wa kata ya Ipera Mhe. Festo Myuguye  ameomba serikali kupimia wananchi maeneo yao na viwanja vyao, ili wananchi waweze kupata fursa ya kutumia hati za viwanja vyao kupata mikopo.

“ tunaomba pia serikali itusaidie kujenga miundo mbinu ya maji katika maeneo ambayo hayajafikiwa na huduma hiyo ili kuwafikia watu wengi, miundo mbinu iliyopo ilijengwa kabla ya Kijiji kuwa kikubwa”

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.