TAARIFA KWA VYOMBO
VYA HABARI
August 30, 2022
TAASISI YA JAKAYA MRISHO KIKWETE
NA UNA TANZANIA ZAANDAA MAFUNZO KUADHIMISHA SIKU YA VIJANA DUNIANI 2022
Kaulimbiu; Mshikamano wa Vizazi: Kuunda Ulimwengu kwa
Vizazi Vyote.
DAR ES SALAAM AGOSTI 30, 2022: Taasisi ya Jakaya
Mrisho Kikwete (JMKF) ikishirikiana na Asasi ya Umoja wa Mataifa (UNA) Tanzania na wadau mbalimbali itakutanisha Jumla ya vijana 150 katika
mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kuimarisha biashara na kazi endelevu za
mashirika ya Vijana mnamo tarehe 2 na 3 Septemba, 2022 katika ukumbi wa
Makumbusho ya Taifa na Nyumba ya Utamaduni mtaa wa Shaaban Robert jijini Dar es
salaam.
Mafunzo hayo, ambayo ni sehemu ya maadhimisho ya siku
ya Vijana duniani (IYD2022), yatakuwa jukwaa la kufichua fursa na rasilimali
kwa vijana ambazo zitasababisha kukuza upatikanaji wa kazi zenye staha na kukuza
ushiriki wao bora kwenye masuala yanayowahusu. Kitaifa maadhimisho haya yalifanyika
tarehe 12 Agosti, 2022 kaulimbiu ikiwa “Kila Mmoja Anahusika Kujenga Uchumi Imara,
Ustawi Na Maendeleo Endelevu: Jiandae Kuhesabiwa”
“Kutakuwa na mafunzo ya kusisimua kutoka kwa wataalam
waliobobea katika sekta binafsi na asasi za kiraia. Mafunzo haya ambayo yameandaliwa
kwa pamoja na vijana, yatatumika kuchochea ujuzi na maarifa, ushauri kutoka kwa
wabobezi katika sekta husika ili
kuongoza mazungumzo baina ya vizazi. Maeneo ya mafunzo yaliyoainishwa
katika programu yalipendekezwa na zaidi ya vijana 50 kutoka sekta binafsi na za
kiraia”,anamasema Mtendaji Mkuu wa JMKF Bi. Vanessa Anyoti.
Bi. Anyoti anaongezea kwamba: “Siku ya Vijana Duniani
imekua jukwaa muhimu la kuthamini mchango mkubwa wa vijana katika kuleta maendeleo ya
kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.
Tanzania inaungana na mataifa mengine Wanachama wa Umoja wa Mataifa
kujadili, kusherehekea na kutambua nafasi ya Vijana katika kuleta maendeleo ya
kiuchumi, kutoa mapendekezo na kuonesha uwezo wa vijana.
Hii, inatokana na ukweli kwamba, vijana ndio kundi
kubwa katika jamii yoyote ile. Vijana ndio wenye nguvu zaidi ya kufanya kazi,
Vijana ni wabunifu, Vijana ndio chachu ya mabadiliko chanya katika jamii na
Vijana ndio walinzi wa historia na warithi wa Mataifa yao”, anafafanua.
Kwa taarifa Zaidi wasiliana na Nicholaus Luoga kupitia
0759506122 na kupitia nicholaus.luoga@jmkfoundation.org
MAELEZO YA MAADHIMISHO KWA
UFUPI
Jina
la Tukio |
|
Tarehe Muda |
2-3
Septemba 2022 Saa
3.00 Asubuhi |
Mahali |
Makumbusho
ya Taifa na Nyumba ya Utamaduni, Dar es Salaam |
Waandaaji |
Taasisi
ya Jakaya Mrisho Kikwete wakishirikiana na UNA Tanzania. |
Wawasilishaji
Mada |
|
Nani
anaweza kushiriki? |
Vijana
150 wanaomiliki biashara na waliokua na asasi za kiraia. |
Lugha
itakayotumika |
Lugha
ya Kiswahili, japo baadhi ya mada zitachanganya lugha kulingana na aina ya
wawasilishaji mada watakaokuwepo. |
No comments:
Post a Comment