Habari za Punde

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Mpango Amefanya Mazungumzo na Katibu Mkuu wa UN New York

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa  Dkt. Philip Mpango akiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mheshimiwa Antonio Guterres kabla ya mazungumzo yao yaliofanyika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa Jijini New York nchini Marekani.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa  Dkt. Philip Mpango akimkabidhi zawadi ya picha ya Mlima Kilimanjaro unaopatikana nchini Tanzania Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mheshimiwa Antonio Guterres mara baada ya mazungumzo yao yaliofanyika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa Jijini New York nchini Marekani.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa  Dkt. Philip Mpango amekutana na kufanya mazungumzo (Tete a tete ) na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mheshimiwa Antonio Guterres , Mazungumzo yaliofanyika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa Jijini New York nchini Marekani.

Hii leo tarehe 22 Septemba 2022 Makamu wa Rais akimwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuhutubia Mkutano wa Baraza Kuu la 77 la Umoja wa Mataifa (UNGA) unaondelea nchini Marekani.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.